STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 10, 2013

MAGDALENA OLOTU AWA REDD'S MISS KIGAMBONI 2013


IMG_0566Mshindi wa Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu (katikati) akila pozi katika picha ya ukumbusho na mshindi wa pili Latifa Mohamed( wa pili kushoto) na Mshindi wa tatu Irene Rajab ( wa pili kulia) pamoja na mshindi wa nne na wa tano.
IMG_0570
IMG_0588Mgeni rasmi katika shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Mbunge wa jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile (CCM) akitoa nasaha zake kwa mshindi wa taji la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu mara baada ya kuibuka kidedea wa taji hilo ambapo amemtakia Baraka zote kuiwakilisha vyema Kigamboni.
IMG_0596Mgeni rasmi katika shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Mbunge wa jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile (CCM) akimkabidhi zawadi ya fedha taslimu shilingi 500,000/mshindi wa taji la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu iliyotoka mfukoni kwa Mbunge huyo.
IMG_0601Meneja Masoko Taifa wa shirika la ndege la Precision Air Bw. Ibrahim Bukenya akikabidhi zawadi ya fedha taslimu shilingi 250,000/ kwa mshindi wa tatu wa Redd’s Miss Kigamboni 2013 Irene Rajab.
IMG_0605Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Bw. Prashant Patel katika pozi na mshindi wa pili wa shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Latifa Mohamed mara baada ya kumkabidhi zawadi ya fedha taslim shilingi 300,000/.
IMG_0612Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu katika pozi na kitita chake cha fedha taslim shilingi 500,000/ zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile( na FullshangweBlogu)

Mengi awaonya wanaowania Urais 2015



MWENYEKITI wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.

Mengi ameyatoa maombi yake ya m
oyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia.

Chanzo: Upekuzi Huru

Washindi wa tuzo za Kili Music Awards 2013 hawa hapa



Add caption









WIMBO BORA WA RNB; RAMA DEE ft MAPACHA-KUWA NA SUBIRA

KIKUNDI BORA CHA TAARABU-JAHAZI MODERN TAARAB

MTUNZI BORA WA TAARABU-THABIT ABDUL

WIMBO BORA WA TAARABU;KHADIJA KOPA-MJINI CHUO KIKUU

MTAYARISHAJI WA WIMBO WA MWAKA KWA TAARABU-ENRICO


MSANII BORA WA KIKE -TAARBU; ISHA MASHAUZI

MSANII BORA WA KIUME -TAARABU; MZEE YUSUPH

WIMBO WENYE VIONJO VYA ASILI-MRISHO MPOTO ft DITTO-CHOCHEENI KUNI

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI BONGO FLAVA-BEN POL

MTAYARISHAJI BORA WA MWAKA-MUZIKI WA KIZAZI KIPYA; MAN WALTER

MSANII BORA WA KIUME BONGO FLAVA-DIAMOND
MSANII BORA WA KIKE BONGO FLAVA-RECHO

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI HIP HOP-KALA JEREMIAH

WIMBO BORA WA BONGO POP;OMMY DIMPOZ-ME AND YOU

MSANII BORA ANAYECHIPUKIA-ALLY NIPISHE

MSANII BORA WA KIUME-DIAMOND

KIKUNDI BORA CHA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA-JAMBO SQUAD

MTAYARISHAJI CHIPUKIZI WA MWAKA-MENSEN SELECTA

WIMBO BORA WA BENDI;MASHUJAA-RISASI KIDOLE

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI -BENDI; CHARLS BABA

MTAYARISHAJI WA WIMBO WA MWAKA-BENDI ;AMOROSSO

MSANII BORA WA KIKE-BENDI ;LUIZA MBUTU

MSANII BORA WA KIUME-BENDI ;CHARLS BABA

BENDI BORA YA MWAKA-MASHUJAA BAND

WIMBO BORA WA ZOUK; AMINI -NI WEWE

WIMBO BORA WA REGGAE;WARRIORS FROM THE EAST-KILIMANJARO

WIMBO BORA WA RAGGA/DANCEHALL; DABO-PREDATOR

MSANII BORA WA HIP HOP-KALA JEREMIAH

WIMBO BORA WA HIP HOP; NAY WA MITEGO-NASEMA NAO

WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI;JOSE CHAMELEONE-VALUVALU

WIMBO BORA WA KUSHIRIKIANA;OMMY DIMPOZ ft VANESSA-ME AND YOU

WIMBO BORA WA MWAKA; KALA JEREMIAH-DEAR GOD

VIDEO BORA YA MWAKA;OMMY DIMPOZ-BAADAE

HALL OF FAME-KILIMANJARO BAND WANA NJENJE

HALL OF FAME-SALUM ABDALLAH YAZIDU

MSANII BORA WA KIKE-LADY JAY DEE



KASEBA ALIVYOMSAMBARATISHA SIMWANZA WA MALAWI

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Ibrahimu Maokola kushoto akioneshana kazi na
JOSEPHER NJELEKELA(KAMANDA WA KAMANDA) wakati wa mpambano wao Maokola alishinda kwa KO ya raundi ya tatu
Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Juma Fundi akioneshana umwamba na Moro Best wakati wa mpambano huo

Bondia Juma Fundi akioneshana umwamba na Moro Best wakati wa mpambano huo
Juma fundi alishinda kwa KO raundi ya sita

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Japhet Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Rasco Simwanza wa Malawi wakati wa mpambano wao wa Ubingwa wa Kimataifa wa PST mpambano uliofanyika Dar es salaam jana Kaseba alishinda kwa TKO ya raundi ya tano Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Rasco Simwanza kutoka Malawi kushoto akipambana na Japhet Kaseba wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa Kimataifa wa PST kaseba alishinda raundi ya tano

Bondia Japhet Kaseba akiwa amevishwa mkanda wake wa kimataifa wa PST

Bondia Kaseba akishangilia ushindi zaidi tembelea www.superdboxingcoach.blogspot.com

Watanzania wang'ara katika mbio nchini Kenya

KATIKA kuhakikisha riadha nchini Tanzania inafuta uteja kwa wakimbiaji
wake kwa wafukuza upepo wa Kenya, Klabu ya Holili (HYAC) ya Mkoani
Kilimanjaro imedhihirisha hilo katika Taveta Athletics Championship
kwa kuwabwaga Wakenya katika mbio za meta 5000, 1500, 800 na 100.

Michuano hiyo ya Taveta imefanyika mwishoni mwa wiki katika Kaunti ya
Taita-Taveta katika Mkoa wa Pwani nchini Kenya katika wilaya ya Taveta
kwa kuwakutanisha wanariadha wa nchini Kenya huku Holili Youth
Athletics Club ikialikwa kutoka nchini Tanzania.

Katika Mbio za meta 5,000 alikuwa ni Baraka Williams aliyekimbia kwa
dakika 14:45:22 nafasi ya pili ikishikwa na Mtanzania mwingine
Abubakar  Joel aliyekimbia kwa muda wa 16:00:00  na nafasi ya tatu
ikashikwa na Mkenya Kivoko Makao ambaye alikimbia kwa muda wa
16:34:00.

Wambura Lameck, Mtanzania kutoka katika klabu ya Riadha kwa vijana
(HYAC) alionyesha uwezo katika mbio za meta 100 na 800 kwa wanaume;
katika mbio za meta 100 Wambura alikimbia kwa muda wa sekunde 12:67
akiwatupa Wakenya Walter Kamujalo (13:12), Emmanuel Paulo (13:70) na
Joseph Daudi (14:20).

Mbio za mita 800 Wambura Lameck alikimbikia kwa muda wa dakika 2:02:16
akimwacha Mkenya Ropya Nyingi ambaye alichukua muda wa dakika 2:04::14
na nafasi ya Tatu ikishikwa na Mtanzania kutoka HYAC Paulo Jackson
aliyekimbia kwa muda wa dakika 2:05:98, Wakenya wengine Joseph Daudi
(3:00:00) na Philip Matheka (3:04) walisshika nafasi mbili za mwisho.

Pia Watanzania waliwaonyesha kazi nyingine Wakenya katika mbio za meta
1500 pale Baraka Williams kutoka HYAC alipowakimbiza na kuongoza baada
ya kumaliza kwa muda wa dakika 3:48:77 akifuatiwa na Mkenya Vicent
Daniel kutoka Taveta aliyemaliza kwa kutumia muda wa dakika 4:16:85
nafasi ya tatu ikishikwa na Mtanzania mwingine kutoka HYAC Paulo
Jackson ambaye alikimbia kwa dakika 5:04:66 na Mkenya Tumuna Ludovick
akikimbia kwa muda wa dakika 5:09:07.

Kwa upande wa wanawake Watanzania Furaha Sambeke na Pendo Pamba
walifanya kweli katika meta 800 kwa kushika nafasi mbili za juu.

Furaha Sambeke anayenolewa na Klabu ya Holili Youth Athletics
alikimbia kwa muda wa dakika 2:30:00 na Pendo Pamba akimaliza kwa
dakika 3:10, nafasi ya tatu ilishikwa na Mkenya Emily Wamboi na ya nne
ikishikwa na Mkenya mwingine Cecily Kimale ambao wote walikimbia kwa
kuda wa dakika 3:22:00 na 4:12:00.

Taveta Athletics Championship imefanyika ikiwa na makusudi ya
kutengeneza Timu ya Riadha ya Taifa la Kenya ambako mchujo rasmi
utafanyika Mjini Mombasa kwa watanzania walioshinda katika mbio hizo
nao watakuwemo katika kinyang’anyiro hicho kwa ajili ya kupata uzoefu
zaidi kutokana na ukweli kwamba taifa la Kenya limekuwa bora katika
riadha barani Afrika.

Mwandishi: Johnsona Jabir, Moshi-Kilimanjaro