STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 10, 2013

Swagger One aangusha tatu kwa mpigo

Swagger katika pozi
Filamu ya Jeshi la Mfu itakayoanza kutolewa kabla ya nyingine

Kava la filamu ya Salamu Toka Kuzimu
Muonekano wa filamu ya Katikati ya Jiji

MSANII wa zamani wa muziki wa kizazi kipya aliyejitosa kwenye uongozaji wa filamu, Hussein Ramadhan 'Swagger One' amerekodi filamu mpya tatu kwa mpigo za 'Jeshi la Mfu', 'Sauti Toka Kuzimu' na 'Katikati la Jiji'.

Akizungumza na MICHARAZO, Swagger aliyetamba na makundi ya Double W na Crime Busters, alisema filamu ya kwanza kutoka kati ya hizo ni 'Jeshi la Mfu' itakayofuatiwa na 'Sauti Toka Kuzimu' na kisha 'Katikati ya Jiji' inayozungumzia maisha halisi ya biashara ya miili inayofanywa na baadhi ya wanajamii nchini.

Alisema filamu zote hizo zimewashirikisha wasanii mchanganyiko wakiwamo wenye majina na chipukizi kwa lengo la kutoa ladha tofauti na pia ni kati ya filamu anazotarajia zitaleta mapinduzi katika tasnia hiyo kutokana na simulizi zake.

"Ni filamu za aina yake, sijisifu kwa vile nimeziandaa, ila ukweli ndivyo ulivyo siyo filamu za sebuleni na kulilia mapenzi, ni kazi za kusisimua ambazo tumezoea kuziona kwa watayarishaji na waongozaji wa kimataifa duniani," alisema.

Mtayarishaji huyo aliongeza kuwa amekuja na filamu za kusisimua ili kuondoa dhana kwamba soko la filamu limetekwa na masimulizi ya mapenzi tu.

"Nimekuja tofauti ili kuwapa fursa wasiofagilia filamu za kimapenzi wapate ladha nyingine ya kusisimua hasa hii ya 'Sauti Toka Kuzimu' au 'Jeshi la Mfu' ni kama filamu zile zinazozalishwa Hollywood kwa simulizi na mandhari zake, watu wasubiri kuziona," alisema Swagger.

Kabla ya kujitosa kwenye utayarishaji wa filamu, Swagger alianza kuigiza akishirikiana na mama yake aliyekuwa nyota wa michezo wa kuigiza sambamba na akina Mzee Majuto, Mzee Small, marehemu Mwanachia n Qudrat Olomoda maarufu kama 'Chombeza'.

Wakazi Moro waichoka CCM warejesha kadi




Baada ya kutoa hotuba nzito na zenye kugusa matatizo ya wananchi, wananchi hao walirudisha kadi zao na kwa kuwa kadi hizo lissu hakuja nazo akazichoma moto.

Credit:Mpekuzi Huru

MAGDALENA OLOTU AWA REDD'S MISS KIGAMBONI 2013


IMG_0566Mshindi wa Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu (katikati) akila pozi katika picha ya ukumbusho na mshindi wa pili Latifa Mohamed( wa pili kushoto) na Mshindi wa tatu Irene Rajab ( wa pili kulia) pamoja na mshindi wa nne na wa tano.
IMG_0570
IMG_0588Mgeni rasmi katika shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Mbunge wa jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile (CCM) akitoa nasaha zake kwa mshindi wa taji la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu mara baada ya kuibuka kidedea wa taji hilo ambapo amemtakia Baraka zote kuiwakilisha vyema Kigamboni.
IMG_0596Mgeni rasmi katika shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Mbunge wa jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile (CCM) akimkabidhi zawadi ya fedha taslimu shilingi 500,000/mshindi wa taji la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu iliyotoka mfukoni kwa Mbunge huyo.
IMG_0601Meneja Masoko Taifa wa shirika la ndege la Precision Air Bw. Ibrahim Bukenya akikabidhi zawadi ya fedha taslimu shilingi 250,000/ kwa mshindi wa tatu wa Redd’s Miss Kigamboni 2013 Irene Rajab.
IMG_0605Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Bw. Prashant Patel katika pozi na mshindi wa pili wa shindano la Redd’s Miss Kigamboni 2013 Latifa Mohamed mara baada ya kumkabidhi zawadi ya fedha taslim shilingi 300,000/.
IMG_0612Redd’s Miss Kigamboni 2013 Magdalena Olotu katika pozi na kitita chake cha fedha taslim shilingi 500,000/ zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mh. Dr. Faustine Ndugulile( na FullshangweBlogu)

Mengi awaonya wanaowania Urais 2015



MWENYEKITI wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.

Mengi ameyatoa maombi yake ya m
oyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia.

Chanzo: Upekuzi Huru

Washindi wa tuzo za Kili Music Awards 2013 hawa hapa



Add caption









WIMBO BORA WA RNB; RAMA DEE ft MAPACHA-KUWA NA SUBIRA

KIKUNDI BORA CHA TAARABU-JAHAZI MODERN TAARAB

MTUNZI BORA WA TAARABU-THABIT ABDUL

WIMBO BORA WA TAARABU;KHADIJA KOPA-MJINI CHUO KIKUU

MTAYARISHAJI WA WIMBO WA MWAKA KWA TAARABU-ENRICO


MSANII BORA WA KIKE -TAARBU; ISHA MASHAUZI

MSANII BORA WA KIUME -TAARABU; MZEE YUSUPH

WIMBO WENYE VIONJO VYA ASILI-MRISHO MPOTO ft DITTO-CHOCHEENI KUNI

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI BONGO FLAVA-BEN POL

MTAYARISHAJI BORA WA MWAKA-MUZIKI WA KIZAZI KIPYA; MAN WALTER

MSANII BORA WA KIUME BONGO FLAVA-DIAMOND
MSANII BORA WA KIKE BONGO FLAVA-RECHO

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI HIP HOP-KALA JEREMIAH

WIMBO BORA WA BONGO POP;OMMY DIMPOZ-ME AND YOU

MSANII BORA ANAYECHIPUKIA-ALLY NIPISHE

MSANII BORA WA KIUME-DIAMOND

KIKUNDI BORA CHA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA-JAMBO SQUAD

MTAYARISHAJI CHIPUKIZI WA MWAKA-MENSEN SELECTA

WIMBO BORA WA BENDI;MASHUJAA-RISASI KIDOLE

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI -BENDI; CHARLS BABA

MTAYARISHAJI WA WIMBO WA MWAKA-BENDI ;AMOROSSO

MSANII BORA WA KIKE-BENDI ;LUIZA MBUTU

MSANII BORA WA KIUME-BENDI ;CHARLS BABA

BENDI BORA YA MWAKA-MASHUJAA BAND

WIMBO BORA WA ZOUK; AMINI -NI WEWE

WIMBO BORA WA REGGAE;WARRIORS FROM THE EAST-KILIMANJARO

WIMBO BORA WA RAGGA/DANCEHALL; DABO-PREDATOR

MSANII BORA WA HIP HOP-KALA JEREMIAH

WIMBO BORA WA HIP HOP; NAY WA MITEGO-NASEMA NAO

WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI;JOSE CHAMELEONE-VALUVALU

WIMBO BORA WA KUSHIRIKIANA;OMMY DIMPOZ ft VANESSA-ME AND YOU

WIMBO BORA WA MWAKA; KALA JEREMIAH-DEAR GOD

VIDEO BORA YA MWAKA;OMMY DIMPOZ-BAADAE

HALL OF FAME-KILIMANJARO BAND WANA NJENJE

HALL OF FAME-SALUM ABDALLAH YAZIDU

MSANII BORA WA KIKE-LADY JAY DEE