STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 28, 2014

Mourinho aomba radhi kwa kumuuza Mata kwa Mashetani

Mourinho akiwa na Mata enzi wakiwa pamoja Chelsea
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho ameomba msamaha kwa uamuzi wake wa kumuuza Juan Mata Manchester United na kuweka wazi kuwa "ulikuwa uamuzi mgumu" kumuacha kiungo huyo raia wa Hispania kujiunga na mahasimu wao hao wa Old Trafford.
Mata, 25, ameweka rekodi United ya uhamisho baada ya kujiunga nayo kwa paundi milioni 37 akitokea Chelsea, ambako alikuwa hana raha tangu kocha huyo wa kireno kutua Stanford Bridge..
Mourinho aliiambia BBC Radio 5  kuwa angelipenda kuendelea kuwa na Mata katika kikosi chake.
"Kuna uamuzi ambao kocha anatakiwa kuchukua, lakini kwangu mimi ulikuwa uamuzi mgumu. Ningependa kuwa naye katika kikosi changu," alisema Mourinho.
"Mata ni mfungaji mzuri, lakini kuwa na mchezaji katika hali kama hii ni ngumu. Alistahili hilo kwa Chelsea kumfungulia mlango [akapate nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza].
"Ninapenda watu kuwa na furaha. Naomba msamaha sikuweza kumfanya kuwa na furaha katika kikosi hiki - Nimeumia sana katika hilo, lakini ninajenga timu yangu kwa kumchezesha Oscar kama namba 10."
Pia Mourinho alisema pindi Mata atakaporejea Stamford Bridge akiwa na United atamhakikishia mapokezi mema kutoka kwa mashabiki wa Chelsea.
"Ni wa kipekee sana. Nadhani ni 'mchezaji ambaye atabaki kuwa rohoni mwa mashabiki' na pia katika kizazi hiki," aliongeza Mreno huyo.
"Nimekuwa naye kwa kipindi cha miezi sita tu na nilimpenda sana. Sasa chukulia kwa watu ambao wamekuwa naye kwa miaka mitatu. Atabaki kuwa katika historia ya klabu - ametwaa makombe muhimu na watu wanampenda.
"Siku moja atakuja hapa akiwa na jezi ya Manchester United na watu watamuonyesha upendo huo." 

Mashindano ya Ngumi Ilala yaanza

Bondia Husein Pendeza  wa Klabu ya Ashanti Ilala kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde kiufundi na Ayubu Ibrahimu wa Green House wakati wa ufunguzi wa mashindan ya  wazi mkoa wa Dar es salaam yanayoenderea katika ukumbi wa panandi pasnandi Ilala Bungoni Ibrahimu alishinda kwa point 
Mwenyekiti wa Ngumi za Ridhaa Mkoa wa Dar es salaam DABA akimkabidhi risara Mbunge wa Ilala Mussa Azan Zungu wakati wa mashindano ya wazi yaliyoanza jumatatu

Bondia Husein Pendeza  wa Klabu ya Ashanti Ilala kulia  akimtupiana makonde kiufundi na Ayubu Ibrahimu wa Green House wakati wa ufunguzi wa mashindano ya wazi mkoa wa Dar es salaam yanayoenderea katika ukumbi wa panandi pasnandi Ilala Bungoni Ibrahimu alishinda kwa point
 Mbunge wa Ilala Mussa Zungu akifatilia mchezo wa ngumi
Na Mwandishi Wetu

SHILIKISHO la ngumi za ridhaa Mkoa wa Dar es salaam umezindua rasmi mashindano yake ya kwanza tanga waingie Madarakani mashindano hayo yalifunguliwa jumatatu na mgeni rasmi


Mbunge wa Ilala Mussa Azan Zungu ambayo imekutanisha zaidi ya timu ishirini na mabondia 60 wa mkoa huu akisoma risala kwa mgeni rasmi 


Mwenyekiti wa ngumi mkoa wa Dar, Akaroli Godfrey amesema mbali na mashindano hayo kuwa na changamoto mbalimbali wameamua kuyafanya kwa kuwa yapo kwenye karenda yao ata hivyo akuna zawadi zozote kwa mabondia watakaopigana hivyo kama mbunge wa jimbo la ilala tunaomba utupatie angarau medali kwa mabondia aidha vifaa tulivyo navyo avikizi kimchezo


akijibu risara hiyo mbunge huyo ame haidi kutoa zawadi pamoja na kuwa mlezi wa ngumi za ridhaa mkoa wa Dar es salaam na kuwasaidia kutafuta wadhamini mbalimbali watakaojitokeza kuinua mchezo wa masumbwi nchini ili ngumi zisonge mbele 


katika ufunguzi huo mabondia Anton Idoa alimtwanga kwa K,O ya raundi ya pili bondia Mohamed Mzeru huku John Cristian akimsambaratisha Omar Said, na shabani Alimasi akimdunda Saidi Kondo na bondia pekee kutoka timu ya shanti ya Ilala,Hussein Pendeza alipoteza kwa pointi na Ayubu Ibrahimu