STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

HiviI ndivyo hali ilivyokuwa mvua za jana jijini Dar, 10 wafa

Mafuriko kila kona

Baadhi ya nyumba zikiwa zimefurika maji ya mvua zinazoendelea kunyesha Dar
Maisha haya mpaka lini?
Uokozi ulikuwepo Dah! Jiji la Dar Nouma
Uokozi na uopoaji wa waliosombwa na maji
Maji kila kona
Kubebana nako kulikuwapo
Kariakoo Jijini Dar hali ya mvua ipo hivi... ni hatari tupu
Foleni nayo usiombeeeeeeeeeeee....

Sehemu ya maduka yaliyopo eneo la Kituo cha daladala cha ITV yakiwa yamezingirwa na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam. Kutokana na mvua hizo na maji kujaa kumesababisha msongamano mkubwa wa magari kuanzia jana jioni na leo.
 Barabara ya kuelekea Goba....
 Barabara ya Goba ikiwa imeharibika kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
 Maji yakitiririka kwa kasi katika Mto Mbezi eneo la Bondeni...
 Vijana wakitumia fursa vizuri kwa kujipatia mchanga unaotiririshwa na maji ambapo huwauzia madereva wa maroli.
 Eneo la Mwenge karibu na kituo cha daladala.....
 Moja ya daladala lililokuwa gereji likiwa limezingirwa na maji eneo la Mwenge....
 Maduka ya Mwenge yakiwa yamezingrwa na maji.....
 Mdada huyu alikuwa akipiga hesabu na kujiuliza jinsi ya kuvuka maji yaliyojaa na kukatiza barabara eneo la ITV.
 Mwenge karibu na Zahanati...... hakuna njia ya kuingilia Zahanati
 Maduka eneo la Mwenge yamejaa maji....
 Kazi haifanyiki leo katika maduka haya...
 Mwenge eneo la Nakiete......
 Maji yakikatiza barabara eneo la ITV.

MVUA kubwa ziliuzonyesha mfululizo kwa siku ya juzi mpaka leo hii imedaiwa kusababisha vifo vya watu 10 na maelfu kukosa makazi katyika maenepo mbalimbali ya jijini Dar na mkoani Morogoro.

Nani wa kumzuia Tambwe asitwae kiatu cha Dhahabu?

Amissi Tambwe
Na Rahim Junior
AMISSI Tambwe anacheeka! Kufuatia kushuhudia washambuliaji wa timu pinzani katika Ligi Kuu Tanzania Bara wakishindwa kumfikia kileleni kwenye orodha ya Ufungaji Bora licha ya kutoshuka dimbani katika mechi kadhaa kutokana na majeruhi aliyonayo.
Rais huyo wa Burundi anaongoza mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu akiwa na magoli 19, sita zaidi na ya Mfungaji Bora wa msimu wa mwaka jana, Kipre Tchetche anayemfukizia kwenye nafasi ya pili akiwa na mabao 13.
Tambwe aliyenyakuliwa na Simba msimu huu akitokea Vital'O, baada ya kunyakua kiatu cha Dhahabu cha Kombe la Kagame, amewaacha mbali pia nyota wa Yanga wanaofuatia katika orodha hiyo ya ufungaji bora.
Mrisho Ngassa aliyefunga hat trick wiki iliyopita Yanga ilipoizamisha JKT Ruvu pamoja na Hamis Kiiza 'Diego' wana mabao 12 kila mmoja, huku mchezaji aliyeshika nafasi ya pili msimu uliopita Didier Kavumbagu akiwa na magoli 11 sawa na Elias Maguli na ligi ikielekea mwisho.
Kuna kila dalili kwamba Tambwe atanyakua kiatu hicho, labda tu itokee miujiza kwa akina Kipre Tchetche, Ngassa, Kiiza na Kavumbagu wafunge kapu na mabao katika mechi za raundi mbili zilizosalia zikiwemo za leo na zile za kufungia msimu Jumamosi ijayo.
Wafungaji Bora:
19- Tambwe Amisi (Simba)
13- Kipre Tchetche (Azam),
12- Mrisho Ngassa, Hamis Kiiza (Yanga),
11- Didier Kavumbagu (Yanga), Elias Maguri (Ruvu Shooting)

Mvua yapeperusha pambano la Miyeyusho, Cheka PTA

Miyeyusho na mpinzani wake juzi walipopima uzito kabla ya mechi yao kuahirishwa jana kwa sababu ya mvua
MVUA kubwa iliyonyesha kwa siku mbili mfululizo jijini Dar es Salaam, limesababisha kulipeperusha pambano la ngumi la kimataifa kati ya mabondia wa Tanzania, Francis Miyeyusho dhidi ya Mthailand Sukkasem Kietyngyuth lililokuwa lifanyika usiku wa jana kwenye ukumbi wa PTA.
Siyo pambano hilo tu, bali hata pambano jingine la kimataifa baina ya bingwa asiyepigika nchini, Francis Cheka dhidi ya Gavad Zohrehvand wa Iran nalo lilishindwa kufanyika kwa sababu hizo hizo na sasa waratibu wanajipanga kutangaza tarehe mpya, japo imedaiwa michezo hiyo itachezwa mwishoni mwa wiki hii.
Waratibu wa michezo hiyo isiyokuwa ya ubingwa iliyoandaliwa chini ya Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) walitangaza kuahirisha pambano hilo majira ya saa 1 usiku baada ya kutishwa na mvua iliyokuwa imejesha kutwa nzima ya jana bila kukoma.
Hata hivyo mvua hizo zilikoma majira ya saa tatu wakati mashabiki wakiwa wameshatawanyika na hivyo kujipanga kuangalia namna michezo hiyo ifanyike lini ili kuzima kiu ya mashjabiki waliokuwa wana hamu ya kuona mabondiawa Tanzania wangefanya nini dhidi ya wageni hao.