STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

Dogo Rama ndivyo alivyo nje ya Twanga Pepeta

Dogo Rama akiwa katika pozi

MTUNZI na muimbaji wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Ramadhani Athuman 'Dogo Rama' anajiandaa kufyatua albamu ya pili binafsi baada ya albamu ya ile ya kwanza ya 'Kilomita 10,000' kufanya vema sokoni.
Akizungumza na MICHARAZO, Dogo Rama ambaye pia ni rapa wa bendi hiyo alisema mpaka sasa tayari ameshakamilisha nyimbo tatu, mmoja ukiwa umetolewa video yake.
Alizitaja nyimbo hizo zilizokamilika kuwa ni 'Chuki Bila Sababu' alioutolea video akiwa ameimba kwa kuwashirikisha Nyoshi El Saadat, Isha Ramadhan 'Isha Mashauzi', Barnaba na Papi Catalogue, 'Ndivyo Nilivyo' na 'Umaskini Wangu'.
Mwanamuziki huyo aliyekuwa jijini Mwanza kumuuguza mwanae, alisema anatarajia kufikia katikati ya mwaka huu atakuwa ameishakamilisha albamu hiyo nzima aliyopanga iwe na nyimbo zisizopungua nane.
"Nipo katika maandalizi ya kupakua albamu yangu ya pili binafsi itakayochukua nafasi ya 'Kiliomita 10,000 na tayari nimesharekodi nyimbo tatu mpaka sasa," alisema.
Alisema kama ilivyokuwa albamu yake ya awali, albamu ijayo amepanga kushirikisha vichwa mahiri vya muziki wa dansi nchini kwa nia ya kuipa ladha nzuri na tofauti ili kuifanya albamu hiyo iwe ya kipekee.
"Kama ilivyokuwa albamu iliyopita, hii nimepanga kuwashirikisha wanamuziki nyota tofauti ili kuipa ladha zaidi, lengo likiwa kukonga nyoyo za maashabiki wangu," alisema.
Mkali huyo aliyewahi kuzipigia bendi kama Tabora Matata, Msuka na Mwanza Carnival kabla ya kutua Twanga, aliongeza kuwa ana nyimbo zaidi ya tatu kwa ajili ya albamu ya bendi inayotamba na albamu ya 'Shamba la Twanga'.

No comments:

Post a Comment