STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

Simba yavuna ilichopamba, Azam haoooooooooo!

Kikosi cha Simba kilichoaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika

MABINGWA wa soka nchini Simba jana ilikiona cha moto baada ya kutandikwa mabao 4-0 na wenyeji wao Libolo na kuiaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, wakiwaacha wawakilishi wa Kombe la Shirikisho Azam ikipeta kwa kupata ushindi wa mabao 5-0 Sudan Kusini dhidi ya Al Nasir Juba.
Simbe imeng'olewa katika michuano hiyo kwa jumla ya mabao  5-0 baada ya kulala nyumbani Tanzania kwa bao 1-0 kwenye mechi ya awali.
Ikicheza bila nahodha wake, Juma Kaseja, Simba ilienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0 kabla ya kufanya mabadiliko yaliyowagharimu kwa kuruhusu mabao mengine matatu yaliyozima ndoto za klabu hiyo kurejea historia ya mwaka 1979 na 2003 katika michuano hiyo.
Katika miaka hiyo Simba iliweza kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 Zambia dhidi ya Mufurila Wanderers waliokuwa wamewafunga uwanja wa nyumbani mabao 4-0 na pia mwaka 2003 walienda kuitoa Zamalek ya Misri kwa penati.
Kikosi cha timu kinatarajiwa kuwasili nchini leo ili kuja kuendelea na mbio zake za kutetea taji lake la Ligi Kuu Tanzania, ambapo Jumamosi wanatarajiwa kuvaana na Coastal Union wanaolingana nao pointi.
Wakati Simba wakiaga kwa aibu, wawakilishi wengine wa Tanzania Bara kwenye michuano ya kimataifa Azam imesonga mbele kwa jumla ya mabao 8-1 baada ya kuisambaratisha Al Nasir Juba ya Sudan Kusini jana kwa magoli 5-0 katika mechi ya marudiano wiki mbili baada ya kuilaza mabao 3-1 jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Azam walioenda Sudan Kusini wakiwa kama wamefuzu yalipachikwa wavuni na nyota wake, Mcha Khamis 'Vialli', aliyefunga mabao matatu, John Bocco 'Adebayor' na Salum Abubakar 'Sure Boy Jr' waliofunga bao moja moja.
Kikosi cha Azam wawakilishi pekee wa Tanzania waliosonga mbele kwenye michuano ya Afrika
 Nao wawakilishi pekee wa Zanzibar katika michuano ya Ligi ya Mabingwa, Jamhuri imeaga kwa aibu michuano hiyo kwa kufumuliwa jumla ya mabao 8-0, baada ya jana kucharazwa mabao 5-0 wiki mbili tangu wafumuliwe kwa mabao 3-0 mjini Zanzibar na timu ya Kedus Giorgis ya Ethiopia.

No comments:

Post a Comment