STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

Azam sasa kuvaana na Waliberia, kurejea leo kishujaa

Wakali wa Tanzania, Azam Fc
USHINDI wa mabao 5-0 iliyopata Azam jana na kuiwesha kuing'oa Al Nasir Juba ya Sudan Kusini kwa jumla ya mabao 8-1 imeifanya klabu hiyo kuweka historia na sasa inatarajiwa kuvaana na tiu ya Barrack Young Controllers Fc ya Liberia  katika mechi yao ya raundi wa kwanza katikati ya mwezi huu.
Azam iliyoshinda mchezo huo wa Sudan Kusini kwa mabao ya Mcha Khamis 'Vialli', aliyefunga mabao matatu na mengine kupitia kwa John Bocco 'Adebayor' na Salum Abubakar 'Sure Boy' itakutana na wapinzani wao klabu iliyoanzisha mwaka 1997.
Wapinzani wao walipata nafasi hiyo baada ya kuing'oa timu ya Johansens ya Sierra Leone kwa jumla ya bao 1-0  baada ya juzi kutoshana nguvu kwa kutofungana wiki tangu BYC II kupata ushindi wa bao 1-0 nyumbani.
Kwa kufuka hatua hiyo Azam imezidi kuweka rekodi katika michuano mikubwa ya kimataifa inayoishiriki kwa mara ya kwanza, kwani ni hivi karibuni tu iliweka rekodi ya kufika fainali za Kombe la Kagame na kutwaa ubingwa wa michuano ya Hisani ya nchini DR Congo.
Klabu hiyo iliyopanda Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2008-2009, ndiyo wawakilishi pekee wa Tanzania waliosalia kwenye michuano ya Afrika baada ya Simba na Jamhuri ya Pemba kung'olewa jana kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika kwa vichapo vya aibu.
Simba wenyewe walinyukwa mabao 4-0 na Recreativo do Libolo ya Angola na hivyo kung'oka kwa mabao 5-0 wakati wenzao walinyukwa mabao 5-0 jana mjini Addis Ababa, Ethiopia na wenyeji wao Kedus Giorgi.
Katika mechi ya awali iliyochezwa visiwani Zanzibar, Jamhuri ilinyukwa mabao 3-0 na hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 8-0.
AAzam inatarajiwa kuwasili leo nchini kishujaa kusubiri kujiandaa na mechi yao ya Ligi Kuu ikiufukuzia ubingwa kwa mara ya kwanza, na pia kwa pambano la kwanza la raundi ya kwanza dhidi ya Barrack Y. C. II ya Liberia mechi itakayochezwa kati ya Machi 15-17.

No comments:

Post a Comment