STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

Muumin aiotabiria makubwa Victoria Sound

Muumin (mwenye shati ya kijani) akiwajibika jukwaani na wanamuziki wa Victoria Sound

UONGOZI wa bendi ya Victoria Sound umetamba kuwa umejiandaa vilivyo kukabiliana na changamoto pamoja na ushindani uliopo kwenye fani hiyo kwa sasa nchini.
Victoria iliyojiimarisha ikiundwa na wanamuziki wakali chini ya rais Mwinjuma Muumin, imedai inatambua muziki wa sasa una ushindani mkubwa, lakini wenyewe wamejiandaa vya kutosha kukabiliana nao.
Muumin alisema bendi yao ilishasoma hali ya upepo na kujipanga na hivyo haiogopi changamoto inazotarajiwa kukabiliana nazo kwani wanajiamini.
Mtunzi na muimbaji huyo aliyewahi kutamba na bendi mbalimbali ndani na nje ya nchi alisema kwa kutambua hali hiyo wapo tayari kwa lolote kuweza kusimama kama zilivyo bendi nyingine zilizozoeleka nchini.
"Hatuna hofu licha ya kuwapo kwa ushindani, Victoria Sound tumejiandaa vya kutosha tukitegemea kazi zetu na wanamuziki tulionao, muhimu mashabiki watupe sapoti wapate burudani waliyoikosa kwa muda mrefu," alisema.
Muumin alisema makali ya bendi yameanza kuonekana kupitia nyimbo walizoachia hewani na zile zilipigwa kwa mara ya kwanza kwenye uzinduzi uliofana wa bendi hiyo uliofanyika siku ya Ijumaa kwenye ukumbi wa Mango Garden, jijini Dar es Salaam.
"Kifupi ni kwamba tumekuja kuwashika, tupo fiti tofauti na watu wanavyofikiria, tuna wasanii wenye vipaji na uwezo mkubwa sambamba na nyimbo kali ambazo tunaamini zitawapa burudani mashabiki wa dansi," alisema Muumin.

No comments:

Post a Comment