STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

Mbishi Real sasa ana mboga saba


MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Fred Kaguo 'Mbishi Real' amevunja ukimya kwa kuachia wimbo mpya uitwao 'Mboga Saba' ambao umeanza kuchezwa hewani tangu mwishoni mwa wiki.
Akizungumza na MICHARAZO, Mbishi aliyewahi kutamba na vibao kama 'Tozi wa Mbagala' alisema wimbo huo mpya ni wa kufungua mwaka 2013 na ni moja ya kazi alizopanga kuzitoa katika mwaka huu.
Mbishi alisema ameachia wimbo huo wakati akitafakari kuitolea video au la kutokana na kukwazwa na mfumo mpya wa urushaji matangazo wa digitali ambao umefanya kazi za wasanii zisitangazike kama zamani.
"Nimeachia wimbo wangu mpya wa 'Mboga Saba' ambao utaanza kusikika hewani Machi 1, pia nipo katika kizungumkuti kama niutolee video au la," alisema.
Baadhi ya kazi za msanii huyo anayejishughulisha na umachinga ni pamoja na 'Business', aliyomshirikisha marehemu Complex, 'Pombe' aliomshirikisha Q Jay , 'Nimesomeka' alioimba na Bwana Misosi na 'Amebaka' alioimba na Chege na Jay Mo.

No comments:

Post a Comment