STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 4, 2013

TOTTENHAM  YAINYUKA ARSENAL, MANCHSTER CITY DIMBANI LEO

Garreth Bale akifunga bao la kwanza la Tottenham katika mechi ya jana


KIKOSI cha vijana wa Andre Villas Boas, Tottenham Hotspur, jana waliendeleza  makali na ubabe kwa klabu za London ya Kaskazini baada ya kuwanyuka wapinzani wa Arsenal kwa mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu ya England.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa White Hart Lane nyumbani kwa Spur, Arsenal ilishtukizwa kwa bao la mapema lililofungwa na Garreth Bale kabla ya Aaron Lennon kuongeza bao la pili dakika mbili kabla ya mapumziko.
Arsenal waliocheza kichovu kipindi cha kwanza na kurejea toka mapumziko walifanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na beki wake 'ngongoti' Mertesacker.
Ushindi huo umeifanya Spur kurejea kwenye nafasi yake ya tatu iliyokuwa inaishikilia kabla ya kuenguliwa Jumamosi na Chelsea waliopata ushindi dhidi ya West Brom kwa bao 1-0.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena usiku wa leo kwa pambano moja la timu za Aston Villa itakayoikaribisha mabingwa watetezi wa Li litakalowakutanisha mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Manchester City waliopo nafssi ya pili.
 

No comments:

Post a Comment