STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 10, 2013

Breaking Newzzz: Muigizaji nyota Kash afariki dunia



Jaji Khamis 'Kashi' enzi za uhai wake

 
Kash enzi za uhai wake
MUIGIZAJI nyota wa zamani wa kundi la Shirikisho Msanii Afrika, Jaji Khamis 'Kashi' amefariki dunia akiwa kalazwa hospitali ya Muhimbili.
Habari iliyotufikia jioni hii  zinasema kuwa Kash alifariki mchana wa leo hospitalini hapo alipokuwa amelazwa .
 Baadhi ya wasanii wenzake wa zamani wa kundi hilo lililotamba na maigizo yake kwenye kituo cha ITV, wamethibitisha kufariki kwa muigizaji huyo ambaye pia alikuwa akicheza filamu.
Kashi alitamba na wasanii wenzake kupitia michezo kama Tamu Chungu, Dumaza, Hatia, Gumbizi na mengine.
Wasanii waliokuwa akiigiza nao kabla ya kundi hilo kuzimika ni pamoja na Bakar Makuka 'Beka', Richard Mshanga 'Bosi Masinde', Samson, Vailet, Grace Mapunda 'Mama Kawele' na wengine.
Mwili wa muigizaji huyo unatarajiwa kuzikwa kesho Jumanne na msiba upo Kinondoni-Mkwajuni jijini Dar es Salaam.
Mungu ailaze roho ya marehemu Kashi mahali Pema Peponi Ameen.

No comments:

Post a Comment