STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 10, 2013

Man City yamtolea macho Al ShaarawySp

Stephan Al Shaarawy
KLABU ya Manchester City inamtolea macho mshambuliaji kinda wa Italia anayeichezea AC Milan, Stephan El Shaarawy, japo mchezaji huyo kuitaka klabu hiyo kufanya kweli kama kweli inamtaka amesisitiza kuwa hafikirii kung'oka katika klabu yake ya sasa.
Habari zilizoripotiwa na gazeti la The Sun linasema kuwa kinda hilo linatakiwa Etihad kwa kitita cha paundi Mil. 30, lakini mwenyewe amenukuliwa akisema hafikirii kuondoka San Sirro.
"Sifikirii kuondoka Milan, iwapo City ni kweli inanihitaji mimi, ifanye hivyo, lakini nataka kubaki AC Milan, Mara zote najihisi kujiamini kwa sapoti ninayopewa na klabu, kocha Massimiliano Allegri na timu nzima," alisema.
"Pia nawashukuru wote kwa kunisaidia kuwepo kwenye timu ya taifa ya Italia," alisema mkali huyo wa mabao.

No comments:

Post a Comment