STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 14, 2013

Langa Kileo kuagwa, kuzikwa Jumatatu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgWGDLQAyXnDjIl54AOfwLOs9GWpx_kuFG4f29mB9PBbQjxKZjvccWU9K8Cq7w-AUdhQdWHuRv5exQJDSPhVY6yrhWNX3yGJjktqAA4RXy7VcT9j55-G2nYKoCMGsdG9eksuyDvsYiVDN5Q/s1600/LANGA+(1).jpg
Langa enzi za uhai wake
MWILI wa msanii Langa Kileo aliyefariki jana jioni unatarajiwa kuagwa siku ya Jumatatu kabla ya kuzikwa siku hiyo kwenye makaburi ya Kinondoni.
Taarifa kutoka kwa familia ya marehemu aliyefia hospitali ya Muhimbili, inasema kuwamwili huo utaagwa rasmi saa 7 ya Juni 17 na jioni yake kuzikwa kwenye makaburi ya Kinondoni na kwamba msiba kwa sasa upo nyumbani kwa wazazi wa marehemu, Mikocheni nyuma ya Hospitali ya AAR.
Langa, aliyeibuliwa na shindano la Coca Cola Pop Stars, akiunda kundi la WAKILISHA sambamba na wasanii Witness na Shaa, alifariki jana baada ya kuumwa ghafla kwa kilichoelezwa malaria ikiwa ni siku chache tangu atambulishe video ya wimbo wake wa 'Rafiki wa Kweli'.
Kifo hicho kimekuja wiki chache pia tangu tasnia ya sanaa nchini hasa muziki kumpoteza mkali mwingine wa hip hop, Albert Mangweha 'Ngwair' aliyefariki Mei 28 akiwa Afrika Kusini.
Mkali huyo anakumbukwa na ngoma zake kali akiwa na kundi la Wakilisha kabla ya kujiengua na kutoa kazi zake binafsi ikiwemo iliyomtangaza vyema ya Kimbia.

No comments:

Post a Comment