STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 14, 2013

Simba yaamua kumtosa Ssenkoomi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh_TiroleOvZDZONKYHK37wThvZ5Uc3cunEt-Jl1CDD3w3ngrOkvo0xDy_j_U5vgSAPSPaJBk9ksk7arJU6Jc4H2G-95XTkqFP2UoMq1F2SX-9RQV2CxK8NM0BSbrDLNXYPfDL8Xk04-o5g/s1600/DSC_0738.jpg
Ssenkoomi (kulia)

KLABU ya soka ya Simba imeamua kuachana na beki Mganda Samuel Ssenkoomi baada ya kutoridhishwa na kiwango chake tangu ajiunge na timu hiyo Juni 4 mwaka huu kwa ajili ya majaribio. 
Habari za uhakika kutoka Simba  zinasema kuwa tayari uongozi umeshamkatia tiketi ya bus la  tayari kumrejesha kwao nchini Uganda.
Kiongozi mmoja wa Simba amesema kwamba Ssenkoomi anatarajiwa kuondoka nchini wakati wowote kuanzia sasa baada ya kushindwa kuonesha kiwango cha kuridhisha tangu atue nchini kwa majaribio. 
Ssenkoomi aliyeanza  kujinoa na wenzake Juni 5 kupitia mazoezi yanayoendelea kwenye uwanja wa Kinesi, ameshindwa kuonesha makali kama ilivyotarajiwa huku kocha mkuu wa Simba Abdallah ‘King’ Kibaden kwa nyakati tofauti alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa haridhishwi na kiwango cha Mganda huyo ambaye alikuwa nakipiga katika klabu ya URA.

No comments:

Post a Comment