STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 14, 2013

United yapania rekodi ya uhamisho kwa Ronaldo au Bale

Bale (kushoto) na Ronaldo (kulia)
KLABU ya Manchester United imepania kuweka rekodi ya dunia ya uhamisho wa wachezaji ikianza maisha bila ya Sir Alex Ferguson.
Wamiliki wa klabu hiyo ukoo wa Glazers wakiwa chini ya meneja mpya, David Moyes na fedha za kutosha imepania kuweka rekodi yta kumsajili ama Cristiano Ronaldo au Garreth Bale.
Ronadlo alifunguka jana kuwa milango i wazi kwake kurejea Old Trafford kwa kuwa alikuwa bado hajasaini mkataba wowote wa kusalia Real Madrid kama ilivyovumishwa awali.
Iwapo winga huyo wa Ureno ataamua kusaini mkataba mpya wa kusalia Bernabeu, basi Moyes atatupia macho yake kwa mchezaji bora wa EPL Bale anayeuzwa na klabu yake kwa kitita cha pauni Mil 85.
Wamiliki hao kutoka Marekani anataka kuifanya klabu yao iendelee kutamba Ulaya hata baada ya Ferguson kustaafu baada ya kuipa mataji lukuki ikiwa chini yake.
Ronaldo, 28, anaendelea kuwa chaguo la kwanza la United linalotupiwa macho na jana Mreno huyo aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter kukanusha taarifa kwamba alikuwa anajiandaa kusaini mkataba mpya.
"Taarifa zote zilizoandikwa juu yangu kuhusu kusaini mkataba mpya ni uongo," aliandika Ronaldo.
Hata hivyo Rais wa Real Madrid, Florentino Perez  ameapa kumbakisha mreno huyo, hali inayoweza kutoa nafasi kwa Bale, 23 kuweka rekodi ya uhamisho iliyowekwa na Ronaldo aliposajiliwa na Real kutoka United miaka miwili iliyopita.
United ilimuuza Ronaldo kwa Real kwa kitita cha pauni Mil 80, lakini kama United itamnyakua Bale anayewindwa pia na Real Madrid na PSG atavunja rekodi ya dunia ya uhamisho.

No comments:

Post a Comment