STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 27, 2013

Mwanamke akamatwa kwa sangoma akidaiwa kupanga mauaji


MWANAMKE aliyetajwa kwa jina la Magreth Simon Nkwera ambaye andaiwa ni mtoto wa kwanza wa Mnadhimu Mkuu wa kwanza wa JWTZ Brig Gen Simon Nkwera amekamatwa kwa Mganga wa kienyeji akijaribu kutekeleza jaribio la mauaji.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimepenyezwa kwa blogu hii pamoja na picha zinasema kuwa mwanamke huyo alifumwa 'live' kwa sangoma akifanya mipango ya kutekeleza mauaji kwa njia ya kishirikina dhidi ya watoto wa mumewe na baadhi ya ndugu zake huko Kibaha Maili Moja, Pwani.
Kwa sasa mwanamama huyo anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha Maili Moja akisubiri kupandishwa kizimbani kwa kosa linalomkabili.
Mtuhumiwa akiwa ndani ya  chumba cha mganga na mganga wake aitwae Yahaya tayari kwa mauwaji
 Mtuhumiwa huyo akiwa ndani ya gari la polisi pamoja na mganga wake aitwae, Yahaya tayari.
 Mtuhumiwa huyo akiwa ndani ya gari la polisi baada ya kukamatwa
Mtuhumiwa akiwa anahojiwa na mzee wa ukoo wa shirima Ofisa Polisi Jeshi daraja la Kwanza (woii mstaafu) Joseph Shirima mara baada ya kumkamata live kwa sangoma.

No comments:

Post a Comment