STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 27, 2013

Tevez atangulia Juve, Kolarov njiani kumfuata

Aleksandar Kolarov and Carlos Tevez - Manchester City v Aston Villa - Capital One Cup Third Round
Kolarov, Tevez wakiwa na Balotelli walipokuwa wote Manchester City
MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Manchester City, Carlos Tevez ametua kwa mabingwa wa Italia, Juventus, huku 'kibibi' hicho cha Turin kikiamini kuwa kitafanikiwa kumchukua Aleksandae Kolarov ili kuichezea klabu yao.
Tevez aliyekuwa akiwindwa na klabu mbalimbali ikiwemo Ac Milan, ametua Juventus na kukabidhiwa jezi namba 10 baada ya kufaulu vipimo vya afya.
Juventus inaamini baada ya kumnyakua Muargentina huyo, mchezaji mwingine atakayetua Turin ni Mserbia Kolarov, 27 aliyesajiliwa na City kwa thamani ya pauni Mil 16 miaka mitatu iliyopita akitokea Lazio ya Italia.
City haijaweka wazi mipango ya kumuachia beki huyo, lakini hiyo tgayari kocha mpya wa timu hiyo  amefua wazi kutokuwa na mpamngo na beki huyo na kutoa nafasi ya kumfuata Tevez Juventus kirahisi.Tevez alinukuliwa akifurahia kutua kwake Juve ambayo msimu huu iling'olewa kwenye hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich.
Mshambuliaji huyo atakuwa mchezaji wa kwanza kuvaa jezi namba 10 tangu ilivyovuliwa na Alessandro del Piero.

No comments:

Post a Comment