STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 14, 2013

Bingwa wa RCL, zitakazopanda FDL kufahamika leo


BINGWA wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) na timu tatu zitakazopanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zinatarajiwa kufahamika leo wakati timu nne zilizofanikiwa kutinga Nusu Fainali za RCL zitakaporudiana katika viwanja viwili tofauti .
Friends Rangers ya jijini Dar es Salaam iliyodunguliwa bao 1-0 na Polisi Jamii ya Mara itakuwa dimba la nyumbani la Azam Complex, Chamazi katika pambano la marudiano ambapo kama itafanikiwa kulipa kisasi na kushinda kwa idadi kubwa itakata tiketi ya kupanda daraja la kwanza.
Mshindi yoyote wa mechi hiyo ya leo inayotarajiwa kuwa ngumu, itaungana na timu mbili zitakazokuwa nazo uwanjani leo kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga kati ya Kimondo Sc ya Mbeya na Stand United Fc ambazo zimeshajihakikisha kupanda daraja ila zinawania ubingwa wa ligi hiyo ya RCL.
Timu hizo mbili za Stand United na Kimondo zitarudiana kuwania ubingwa, huku Kimondo ikiwa mbele kwa ushindi wa bao 1-0 iliyopata katika mchezo wa kwanza uliocherzwa kwenye uwanja wa
Timu hizo sasa zitacheza Jumapili (Julai 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi. Polisi Jamii ilishinda bao 1-0 mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 6 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine ya Mbeya.

No comments:

Post a Comment