STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 14, 2013

Majina ya askari waliokufa Darfur haya hapa!


MAJINA ya Wanajeshi saba wa Tanzania waliokufa kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur yamepatikana.
Askari hao waliokufa ambao walikuwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini Sudan ni Sajenti Shaibu Othman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Pte. Rodney Ndunguru, Pte. Peter Werema na Pte. Fortunatus Msofe.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kwenye mtandao ni kwamba askari hao walizingirwa na waasi hao na kushambuliwa ambapo 7 walikufa na wengine 14 akiwemo askari Polisi wa Tanzania kujeruhiwa na kukimbizwa hospitalini.

Mungu azilaze roho za askari wetu mahali pema peponi, Amina.

No comments:

Post a Comment