STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 19, 2013

Mama atelekeza kichanga kisa wivu wa mapenzi

http://www.varbak.com/images/photos-of-black-babies-nb17527.jpg
Picha hii haihusiani na tukio hilo la kutelekezwa mtoto mjini Tanga
MWANAMKE mmoja mkazi wa eneo la Mtakuja jijini Tanga, aliyetajwa kwa jina la Asha Muhidini, amedaiwa kumtekeleza mtoto wake mchanga wa miezi miwili na kutokomea kusikojulikana kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi dhidi ya mumewe.
Mtonyaji wa habari hizi, Mariam Victor aliyejitambulisha kama mpwa wa mume wa mwanamke huyo, aliiambia MICHARAZO kuwa, mama huyo amekuwa na mzozo kwa muda mrefu na mumewe aliyetajwa kwa jina la Muhidini Mohammed baada ya mwanaume kuzaa nje ya ndoa mtoto mwenye miaka mitano.
Mariam alisema mwanamke huyo alimtelekeza kichanga hicho kwa kumfungia ndani ya chumba wanachoishi na mumewe tangu saa 1 usiku na walikuja kushtuka saa 5 usiku mtoto akilia na mjomba aliporejea kazini.

Aliongeza kuwa Asha amekuwa akipinga mtoto huyo aliyezaliwa kuja kuishi katia familia yao, lakini mumewe alikuwa akipinga akidai hawezi kuiacha damu yake kwa msimamo wa mkewe huyo.
"Mzozo uliosababisha hili jambo ni mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa na Mjomba ambapo kwa muda mrefu amekuwa akipinga na mkazamjomba (Asha) na jana alikuja kumtembelea baba yake na mke akapinga lakini mjomba alishikilia msimamo wake," alidokeza Mariam.
Alisema hawakujua kinachoendelea mpaka walipobaini kuwa mtoto kaachwa pekee yake na mama wa mtoto katoweka na kuanza kumsaka asubuhi hii bila ya mafanikio na kukimbilia ofisi ya serikali ya mtaa wao kuripoti ambapo wameombwa kuwa na subira kuona kama mwanamke huyo atarudi au la.
"Mwenyekiti katuambia tuvute subira na tumlishe mtoto maziwa na ng'ombe wakati tunasubiri mama yake arejee na kama vipi tuangalie ustaarabu mwingine ikiwemo kuripoti Polisi au kuendelea kumtunza mtoto kwa sababu pia hasumbui zaidi ya anapotaka kunyonya tu," alisema Mariam.
Juu ya mjomba wake na tukio hilo alilofanyiwa na mkewe, Mariam alidai hana la kusema kwa vile ni mpole kupita maelezo na kwamba amekubali kilichotokea kwa sababu kichanga hicho ni mwanae na ana wajibu wa kumtunza hasa ikizingatiwa wanapoishi ni nyuma ya familia hivyo kichanga kitaangaliwa.

No comments:

Post a Comment