STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 19, 2013

Mtwara kumekucha! Lori lenye shehena ya mabomba lashambuliwa mawe dereva hoi


Habari zilizotufikia kutoka mjini Mtwara zinasema kuwa Gari lililokuwa limebeba Shehena ya Mabomba ya Kusafirishia gesi kutoka Mjini Mtwara kuelekea Dar limeshambuliwa na mawe na kupelekea dereva wa lori hilo Kujeruhiwa Vibaya. 
Lori hilo lilianza kushambuliwa mara baada ya kuingia katika eneo la Mikindani Manispaa ya Mtwara Mjini na sababu ya kushambulia gari hilo ni katika kile kinachodhihirisha kuwa wana Mtwara bado hawajakubaliana na hoja ya Serikali ya kutaka Kusafirisha Gesi hiyo kwa ajili ya Manufaa ya Nchi. Lori hilo kwa sasa lipo kituo kikubwa cha polisi  Mtwara.
Tukio hilo linatokea ikiwa ni wiki moja tu imepita tokea watu kadhaa kukamatwa na jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kile kinachodaiwa kusambaza waraka wa kuhujumu miundombinu yote ya gesi mara tu serikali itakapoanza utekelezaji wake wa ujenzi wa bomba hilo kupeleka Dar.

Source: Jamii Forum

No comments:

Post a Comment