STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 10, 2013

Mchungaji Mtikila aibuka na jipya sasa


 
Mchungaji Mtikila
Na Suleiman Msuya
MWENYEKITI wa Chama Cha Democratic Party (DP) Mchunga Christopher Mtikila amesema wapo katika hatua za mwisho za kisheria za kufuta mchakato mzima wa kuandaa katiba kwani ni kinyume cha sheria.
Mtikila alibainisha nia yake hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii.
Alisema jamii inaweza kumshaanga hasa kwa ile ambayo haijui kinachofanyika katika mchakato huo ila anaamini kwataweza kutambua baadae nini anachakifanya kwa maslahi ya Watanzania hasa wale wa Bara ambao yeye anawatambua kama Watanganyika.
Mwenyekiti huyo wa DP alisema iwapo Serikali inahitaji kuwepo kwa katiba mpya ni vema muungano ukavunjwa kwanza kwani muungano unaotajwa kuwepo haupo kisheria jambo ambalo limegharimu Taifa kupoteza fedha nyingi bila kujulikana sababu za msingi.
“Ni jambo ambalo litawashangaza watu lakini nataka mtambue kuwa mimi nafanya vitu kwa umakini sana na ndio maanda kesi nyingi ninazofungua nashinda kutokana na ukweli kuwa najua nini nafanya kwa maslahi ya Watanzania naamini kwa hili pia nashinda,” alisema.
Alisema suala la katiba limechukuliwa kisiasa zaidi bila kuangalia uhalali wake hivyo hayuko tayari kuona jamii ikitengenezewa katiba yenye misingi ya watu wachache ambao wanahija kujijengea maslahi yao.
Mtikila alisema mchakato wa katiba alianzisha yeye mwaka 1986 hadi 1988 lakini alipata upinzania kwa kile anachodai kuwa ni upinzania kutoka kwa viongozi ambao walijua kuwa anachokifanya ni haki ya watu wengi.
Alisema ni vema jamii itakatambua kuwa suala la katiba sio la mtu kuunda tume anayoitaka kufanikisha zoezi hilo kwani ni dhahiri kuwa upo uwezekano wa kupata katiba ambayo itakuwa imeegemea katika maslahi yake.

No comments:

Post a Comment