STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 10, 2013

Waziri Kabaka abanwa na vijana


Waziri Kabaka
Na Suleiman Msuya
WAKATI mchakato wa kuundwa katiba mpya ukiwa umefikia hatua ya kupata maoni ya juu ya rasimu ya katiba Baraza la Vijana la Taifa (JUVITA) limeibuka na kumtaka Waziri wa Ajira na Vijana Gaudensia Kabaka na Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Mstaafu Joseph Warioba kuhakikisha Baraza hilo linatajwa kwenye katiba.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiyi wa JUVITA Fahami Mastawilly wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam.
Alisema dhumuni la JUVITA ni kuhakikisha kuwa vijana wa Kitanzania wa kada zote bila kuangalia elimu zao wanakuwa na chombo ambocho kitakuwa kinawawakilisha katika vyombo vya maamuzi.
Mastawilly alisema wanaamini kupata nafasi ya kuonana na viongozi hao wawili kunaweza kusaidia ombi lao kufanyiwa kazi ili kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa ni sehemu muhimu katika nchi na kuondokana na hali ilivyo sasa.
“Jamani ndugu zangu wanahabari kwa muda mrefu tumekuwa tukiomba baraza la vijana kutambulika rasmi katika katiba lakini tunaona kuwa hatusikilizwi hali ambayo hatuwezi kuivumilia tena kwani tunaamini ni haki yetu,” alisema.
Alisema wao kama vijana waanzishili wa harakati hizo wameshindwa ni kwa nini Tanzania haitaki kuweka baraza la vijana ndani ya katiba wakati ipo mifano ya nchi nyingine ambazo mabaraza yapo kama Kenya, Uganda, Urusi, Ujerumani, Uswisi, Costarica na zingine nyingi.
Mwenyekiti huyo wa JUVITA alisema ni vema maoni yatakayotolewa kupitia mabaraza ya Wilaya kwenye rasimu vijana wote bila kuangalia itikadi zao za kisiasa, kidini, kabila na welimu wanatakiwa kuungana na kuwataka wajumbe wa mabaraza kusisitiza kuwa ibara ya 43 ya rasimu kutaja wazi uwepo wa baraza la vijana katika katiba.
Alisema ibara hiyo inatamka kuwa kila kijana ana haki ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na jamii kwa ujumla na kwa mantiki hiyo serikali itawawekea mazingira, hali ambayo vijana wanahitaji kuwa pasomeke kuwa serikali itahakikisha kuwa vijana wanawekewa chombo cha kuwaunganisha na kuwawakilisha katika vyombo vya maamuzi nchini bila kujali itikadi zao.

No comments:

Post a Comment