STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 11, 2013

Mechi ya Stand, Kimondo nayo kupiwa J'2


Na Boniface Wambura
MCHEZO wa  marudiano wa Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Stand United FC ya Shinyanga na Kimondo SC ya Mbeya uliyokuwa uchezwe Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) umesogezwa mbele kwa siku moja.

Timu hizo sasa zitacheza Jumapili (Julai 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Kimondo ilishinda bao 1-0 mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 6 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi nyingine ya ligi hiyo itakuwa kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na Polisi Jamii ya Mara, na itafanyika kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Mwamuzi wa mechi hiyo ni Hans Mabena kutoka Tanga.

No comments:

Post a Comment