STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 11, 2013

Wajumbe mkutano Mkuu wa TFF kuanza kuwasili kesho Dar

Rais Leodger Tenga na Makamu wake, Athuman Nyamlani wakiteta na Musonye wa CECAFA
Na Boniface Wambura
WAJUMBE wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utakaofanyika Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) wanawasili jijini Dar es Salaam kesho (Julai 12 mwaka huu).

Mkutano huo wa marekebisho ya Katiba utakuwa chini ya uenyekiti wa Rais wa TFF, Leodegar Tenga na utafanyika ukumbi wa NSSF Waterfront kuanzia saa 3 kamili asubuhi. Wajumbe wote wa mkutano huo watafikia hoteli ya Travertine.

Pia mkutano huo utahudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa wakiwemo kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA).

No comments:

Post a Comment