STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 11, 2013

Mada Maugo, Benson Mwakyembe kuzipiga Russia

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj254DzVPfok2LZcApNivkvgoTadiEW4ZOogbXkRWC205DrJrbhCJxCGsMxzUdmq63Qe4jvtOGh4415LQlIltnnvbVLAZsCYoXNk78NUZKKnGT67XvAtaShsvYP8YPdyyNB7nZHr_NT6Ak/s400/Mwakyembe2.jpg
Benson Mwakyembe
 
Mada Maugo (kulia) akiwa na Rais wa TPBO-Limited Yasin Abdallah 'Ustaadh'
MABONDIA machachari wa Ngumi za Kulipwa nchini, Mada Maugo na Benson Mwakyembe wanatarajia kuondoka nchini wiki ijayo kwa ajili ya kwenda Russia kupambana na wenyeji wao katika michezo ya kimataifa itakayochezwa mwishoni mwa mwezi huu.
Kwa mujibu wa Rais wa TPBO-Limited, Yasin Abdallah 'Ustaadh' mabondia hao wataondoka Julai 23 ambapo Maugo ataenda kupigana na Movsur Yusupov wakati Mwakyembe yeye ataonyeshana kazi na Apti Ustarkhanov kwenye michezo itakayochezwa kwenye ukumbi wa Trade & Intertainment uliopo mji wa Kasiysk, nchini Russia.
Ustaadh alisema watanzania hao watapigana na Warusi hao katika michezo ya kilo 75 (Super Middle Weight) itakayokuwa na raundi nane kila mmoja.
Rais huyo wa TPBO alisema mpinzani wa Maugo rekodi yake inaonyesha kuwa amecheza mapambano matatu na yote ameshindwa moja likiwa kwa KO wakati mpinzani wa Mwakyemba amecheza mechi mbili na kushinda moja na mwingine kupigwa.
"Pamoja na rekodi ndogo za wapinzani wao, lakini ikumbukwe kuwa mabondia wa Russia na kwingineko Ulaya huwa hawachezi ngumi za kulipwa bila kucheza ngumi za ridhaa na kufikia hatua ya kushiriki michuano ya Olimpiki kwa maana hiyo Maugo na Mwakyembe wakitarajiwe wepesi Russia," alisema Ustaadh.
Ustaadh aliongeza kuwa tayari mabondia hao wa Tanzania wameshaombewa visa za kwenda nchini humo gharama zote zikilipwa na TPBO-Limited na wataondoka nchini wakiongoza na wakala wao kutoka Kenya, Thomas Mutua atakayeondokea Kenya na kukutana na mabondia hao Dubai.

No comments:

Post a Comment