STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 13, 2013

Ilala yaifuata Mjini Magharib Fainali za Copa


TIMU ya Ilala imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya kuivua ubingwa Morogoro katika mechi iliyoamriwa kwa mikwaju ya penalti.

Hadi muda wa kawaida wa mchezo huo uliochezwa leo (Septemba 13 mwaka huu) jioni Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.

Paul Ngowi ndiye aliyeanza kuifungia Ilala dakika ya 30, lakini Morogoro wakasawazisha dakika ya 50 kupitia kwa Omari Sultan. Katika changamoto ya mikwaju ya penalti, Ilala ilipata tatu dhidi ya mbili za Morogoro.

Ilala sasa itacheza fainali na Mjini Magharibi itakayofanyika kesho (Septemba 14 mwaka huu) kuanzia saa 9 alasiri.

Fainali hiyo ya wavulana itatanguliwa na ile ya wasichana kati ya Mwanza na Ilala itakayoanza saa 7 mchana. Mwanza imepata tiketi ya kucheza fainali baada ya leo kushinda nusu fainali ya pili dhidi ya Mbeya kwa mabao 3-0.

Mabao hayo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume yamefungwa na Flora Fulgence dakika ya 47, Emiliana Akuti dakika ya 56 na Yulitha Masamu dakika ya 57.

No comments:

Post a Comment