STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 13, 2013

'Unga' wachelewesha safari ya Mark Band

Rashid Pembe (kushoto) akiwa na mwanamuziki wenzake wa Mark Band

SAKATA la kubambwa kila uchao kwa Watanzania nje ya nchi kwa tuhuma za kujihusiaha na dawa za kulevya limesababisha safari ya Mark Band kwenda Chile na Peru ichelewe kutokana na ugumu wa kuzipata visa za kuingia katika nchi hizo.
Mark Band iliyojikita na kupiga muziki asilia kwenye mahoteli ya kitalii, ilikuwa itimke nchini wiki iliyopita, lakini zoezi la upatikanaji wa visa za kuingia nchini humo kupitia balozi zilizopo Kenya na Afrika Kusini limeichelewesha safari hiyo kwa wakati.
Mkurugenzi wa bendi hiyo iliyoanzishwa mwaka 2006, Rashid Pembe 'Profesa' alisema tangu Tanzania ichafuke kutokana na kukamatwa kwa raia wake wakihusisha na dawa za kulevya imekuwa usumbufu kwa watu wengine kiasi cha wao kucheleweshewa safari yao.
"Yaani kwa sasa hakuna Mtanzania anayeaminiwa anapotaka kwenda nje ya nchi au kuingia katika taifa jingine kwa kudhaniwa ni wale wale wanaojihusisha na dawa za kulevya, hata sisi imekuwa tabu kupata visa kwa wakati na kufanya tukwame kuondoka mapema," alisema.
Hata hivyo, alisema zoezi la kupata visa za kuingia katika nchi hizo wanazoenda kutumbuiza kwa mualiko maalum limekamilika na wanamaliza mambo madogo kabla ya wiki ijayo kuondoka nchini.
"Nadhani tutaondoka wiki ijayo kwani karibu kila kitu kimekaa vyema kwa sasa japo ratiba yetu ilishavurugwa kwa kuchelewa kuzipata visa," alisema.
Kwa siku za karibuni Tanzania imekuwa ikichafuka kimataifa kutokana na baadhi ya raia wake wakiwamo wasanii na wanamichezo kuripotiwa kutiwa mbaroni katika mataifa mbalimbali kwa tuhuma za kujihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Baadhi ya walioripotiwa  kunaswa ni pamoja na video queen na nduguye, Agness Gerald  'Masogange' na Mellisa Erdwad, strika wa zamani wa Simba, Joseph Kaniki na bondia wa ukoo wa Matumla, Mkwinda na Mbwana Matumla mbali na watanzania wengine kadhaa.

No comments:

Post a Comment