STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 13, 2013

Kivumbi cha FDL kuanza kesho, Kawawa Stadium kutumika Kigoma

JKT Kanembwa wakikaguliwa kwenye michuano ya Miaka 50 ya JKT jijini hivi karibuni jijini Dar
PAZIA la Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) linatarajiwa kufunguliwa rasmi kesho katika viwanja tofauti, huku uwanja wa nyumbani wa  Kanembwa JKT ya Kigoma sasa utakuwa Uwanja wa Kawawa badala ya ule wa Lake Tanganyika.

Uamuzi wa kuhamishia mechi hizo Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji umetokana na Uwanja wa Lake Tanganyika kutumiwa na Serikali katika Operesheni Ondoa Wahamiaji Haramu inayoendelea nchini kwa sasa. Uwanja huo hivi sasa unatumika kuhifadhi wahamiaji hao.
 

Kanembwa JKT inaanzia nyumbani kwa kuikaribisha Polisi Tabora. Mechi hiyo itachezwa Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).

Mechi nyingine za kufungua dimba za ligi hiyo kuwania nafasi tatu za kucheza Ligi Kuu msimu wa 2014-2014 ni Burkina Faso na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro, Mkamba Rangers na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, Majimaji na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na Kimondo na Kurugenzi kwenye Uwanja wa CCM Vwawa katika mechi za kundi B.
Mechi nyingine kwa kesho ni Tessema na Green Warriors zitaoneshana kazi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Siku inayofuata (Septemba 15 mwaka huu) Transit Camp na Polisi Dar (Mabatini mjini Mlandizi) wakati mechi nyingine za kundi hilo la A zitakuwa kati ya Villa Squad na African Lyon (Karume) na Ndanda FC na Friends Rangers (Nangwanda Sijaona, Mtwara).

Kundi C ni Polisi Mara na Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United na Mwadui (Kambarage, Shinyanga) wakati Pamba na Toto Africans zitamenyana Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment