
Na Boniface Wambura
TIMU ya Airtel Rising Stars ya Tanzania kwa wavulana na wasichana itakabidhiwa bendera kesho (Septemba 14 mwaka huu) tayari kwa safari ya Nigeria itakayofanyika keshokutwa alfajiri.
Hafla hiyo ya kukabidhi bendera kwa timu hiyo yenye kikosi cha wachezaji 32 itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ndiye atakayekabidhi bendera kwa kikosi hicho.
No comments:
Post a Comment