STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 13, 2013

Waziri Mulugo aahidi Mil 2 kwa Mbeya City wakiitungua Yanga kesho

http://kifltd.files.wordpress.com/2012/01/01_12_enn75u.jpg
Naibu Waziri Philipo Mulugo

Kikosi cha Mbeya City
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSJsNsHjk8oZes4gIRZJMglBDLy-cqJ__Id6KV6ouVjbXYivTnjTaWyCOanYX5Ih6OyrwPaHjkzm8Gxz-fLOi_cbctliSDX9r5rqi82IUo5V_Wg7As77JRaNzSAHzEH_bs5dPA0IN52NbE/s1600/IMG_8317.JPG
Kikosi cha Yanga

NAIBU Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ametanga kutoa dau la Sh Milioni 2 kwa kikosi cha Mbeya City iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga katika pambano lao la Ligi Kuu Tanzania Bara linalochezwa kesho kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Aidha Waziri huyo ameamua kufunga safari kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea mkoani Mbeya kwa ajili ya kuipa sapoti timu hiyo ya Mbeya City katika mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandanda mkoani humo.
Waziri Mulugo alisema amefunga safari hiyo ili kuhakikisha timu hiyo ya Mbeya City inapata ushindi dhidi ya mabingwa watetezi hao, Yanga ambao wameshatangaza vita dhidi ya timu hiyo wakitamba wameenda mkoani humo kuzoa pointi sita zikiwamo tatu za mechi ya leo.
Mechi nyingine ambayo Yanga imetangaza kuipigia hesabu ni ile ya Jumatano dhidi ya Prisons Mbeya iliyoanza ligi hiyo vibaya.
Waziri Mulugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songwe  mkoani humo, alisema kwa vile anaamini Mbeya City ni timu nzuri na iwapo ikipata sapoti itafanya maajabu katika mechi hiyo ya kesho na nyingine za ligi hiyo iliyokuw amesimama kwa wiki mbili mfululizo.
Alisema kutokana na hilo ndilo maana amefunga safari kwenda Mbeya kuisapoti timu hiyo na kuahidi kuwapa Sjh Mil 2 iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga, aliyokiri ni moja ya timu kubwa yenye uzoefu, lakini bado haamini kama inaweza kufua dafu kwa Mbey City katika mechi hiyo.
"Naifahamu Yanga ni timu nzuri yenye wachezaji wazuri, lakini katika mchezo wa Jumamosi naamini kabisa watabugizwa mabao mengi ya Mbeya City, iliyonilazimu kufunga safari kuja kuisapoti ili ishinde na wakifanya hivyo nitawapa Sh. Mil 2 taslim kama zawadi yao," alisema.
Mbeya City inayonolewa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi inashiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kupanda daraja ikiwa na timu nyingine mbili za Rhino Rangers ya Tabora na Ashanti United ya Dar es Salaam na mpaka sasa ina pointi nne kutokana na mechi mbili ilizocheza.
Ilianza kwa kutoka sare ya bila kufungana na Kagera Sugar kabla ya kuicharaza Ruvu Shooting kwa mabao 2-1 katika mechi yao ya mwisho zote zilizochezwa uwanja wa Sokoine kabla ya ligi kusimama kupisha pambano la kimataifa la Taifa Stars dhidi ya Gambia.

No comments:

Post a Comment