STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 30, 2013

Askari abambwa akifanya ngono na mahabusu chooni

Kim akiburuzwa na wezake kwa kosa la kufumaniwa mahabusu chooni
ASKARI Polisi mmoja mwenye cheo cha kati nchini China, Yun Kim anashikiliwa katika kituo kimoja kidogo akituhumiwa kufanya mapenzi na mahabusu mwanamke ambaye ni mke wa askari mwenzake.

Inadaiwa askari huyo alikumbwa na mkasa huo katika kituo kidogo cha polisi katika kitongoji cha Chau, mjini Beijing, ambapo inadaiwa siku hiyo Kim alikuwa zamu ya usiku pamoja na maaskari wengine, ambapo pia mahabusu huyo alikuwa kituoni hapo kwa kosa la utapeli.

Mwanamke huyo ambaye ni mke wa askari ambaye jina lake limehifadhiwa, anadaiwa kuletwa kituoni hapo kwa kosa la kujipatia dola 200 kutoka kwa mama mmoja waliokuwa wakifanya biashara pamoja.

Kutokana na kushindwa kumlipa mama aliyekuwa akifanya naye biashara, mke huyo wa askari alijikuta akifikishwa kituoni akisubiri kufunguliwa mashtata siku iliyofuata.

Imeelezwa kuwa, mama huyo hakutaka mume wake ambaye ni askari polisi kwenye kituo kingine afahamu kama ana kesi ya utapeli, hivyo aliamua kuongea na askari huyo.

Mke huyo wa askari anadai kukiri kumtapeli mama huyo, hivyo alikuwa tayari kwenda kumchukulia pesa hizo nyumbani kwake.

Afande huyo anadaiwa kumshawishi kimapenzi mama huyo ili amruhusu kwenda nyumbani kuchukua pesa anazodaiwa, lakini sharti pia waongozane wote.

Kwa lengo la kuepuka aibu ya kujulikana na mume wake kama amefikishwa polisi kwa kesi ya utapeli, mama huyo mahabusu alikubali kufanya mapenzi kituoni hapo na askari huyo.

Akisimulia zaidi tukio hilo,  askari mwenzake aliyekuwa zamu, alisema aliwafuma wawili hao kwenye choo cha kike wakifanya mapenzi.

Ilikoanzia ni kwamba, walipanga mchezo mahabusu huyo aombe ruhusa kwenda chooni na ndipo kamanda naye akajisogeza chooni kwa siri na kuanza kufanya mapenzi.

Hata hivyo, askari aliyewashtukia baada ya kubaini muda mrefu ukipita bila askari mwenzake aliyemsindikiza chooni kurudi, aliamua kufuatilia na kuwakuta wakiburudika.
Askari huyo pamoja na mwanamke huyo, wanakabiliwa na kesi ya kufanya ngono eneo la kazi, huku mwanamke huyo akiendelea kukabiliwa na kesi yake ya utapeli.

No comments:

Post a Comment