STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 30, 2013

Kombe la Dunia hatimaye latua Tanzania


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, akilifunua Kombe la Dunia la FIFA katika Uwanja wa michezo wa CCM Kirumba mjini Mwanza jana jioni baada ya kulipokea Kombe hilo lililotua nchini kwa mara ya pili, ambapo leo wananchi watapata fursa ya kupiga nalo picha.
 

Rais Kikwete, akilinyanyua Kombe hilo kwa furaha baada ya kuzindua rasmi shambra shambra za ujio wake nchini katika uwanja wa Kirumba jijini Mwanza jana jioni.
 
Rais Kikwete, akifurahia huku akiwa ameliinua Kombe hilo juu kuwaonyesha wananchi waliojitokeza kwenye Uwanja wa Kirumba kulipokea. Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam, leo watapata fursa ya kupiga picha na kombe hilo katika Uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment