STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 30, 2013

Kocha wa Azam atua Bongo, wa Simba kesho (?)

Kocha Omog alipowasili nchini asubuhi ya leo hapa akielekea kwenye gari (Azam FC)

HATIMAYE kocha mkuu mptya wa Azam, Joseph Omog ametua nchini na anatarajia kutambulishwa kwa wanahabari mara baada ya kumalizana na uongozi wa klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kocha huyo kutoka Cameroon na aliyekuwa akiifundisha timu ya AC Leopards ya Jamhuri ya Congo ametua asubuhi ya leo tayari kusaini mkataba wa kuanza kuinoa timu hiyo iliyoachana na Muingereza Stewart John Hall.
Wakati Azam wakimpokea kocha wao, Simba wenyewe inadaiwa kuwa itampokea kocha wake mpya,  Zdravko Logarusickutoka Croatia kesho tauyari kuanza kibarua chake kuchukua mikoba ya King Abdallah Kibadeni anayedaiwa kuelekea Ashanti United.
Kocha huyo alitangazwa na Kaimu Makamu Mwenyekiti , Joseph Itang'are na kupingwa na Mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage, aliyesisitiza kuwa Kibadeni ataendelea kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo kwani hawaoni sababu ya kumuengua kikosini kwa sasa.
Huyu ndiye kocha mpya wa Simba anayeelezwa atatua kesho nchini

No comments:

Post a Comment