STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

MAJINA YA ASKARI WALIOKUFA AJALINI DODOMA HAYA HAPA

Na. Sylvester Onesmo, Jeshi la Polisi Dodoma.
ASKARI polisi watano mkoani dodoma wamefariki dunia papohapo katika ajali ya gari iliyotokea 31/01/2014 majira ya saa 5 usiku katika barabara kuu ya Dodoma – Morogoro eneo la Mtumba Center, Kata ya Mtumba Tarafa ya Kikombo Manispaa ya Dodoma, ambapo gari namba  ya usajili T.770 ABT Toyota Corolla lililokuwa likiendeshwa na Askari mwenye namba H. 3783 PC DEOGRATIUS wa Wilaya ya Kongwa.
Gari hilo lilikuwa likitokea Dodoma mjini likielekea Wilayani Kongwa liligongana uso kwa uso na gari namba T.997AVW Scania Bus mali ya Kampuni ya Mohamed Trans lililokuwa likiendeshwa na JUMA s/o MOHAMED, miaka 38, Mkazi wa Mwanza, likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma na kusababisha vifo kwa askari watano papohapo. 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amewataja Askari hao waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni:-
1.  D.9084 D/CPL. ADOLF S/O MESHACK SILLA mwenye miaka 51, Mgogo.
2.  F.6459 D/C. EVARIST s/o MOSES BUKOMBE mwenye miaka 34, Muha.
3. H.3783 PC. DEOGRATIUS s/o PATRICK MAHINYILA mwenyw miaka 29, Mgogo.
4. WP.10337 PC. JACKLINE d/o AUGUSTINE TESHA mwenye miaka 22, Mchaga.
5.  WP.10382 PC. JEMA d/o JIMMY LUVINGA mwenye miaka 20, Mhehe. 
Wote ni askari Polisi Wilaya ya Kongwa na hakuna abiria aliyeumia katika basi. 
Kamanda MISIME amesema chanzo cha ajali hiyo kulingana na uchunguzi wa awali ni mwendo kasi kutokana na uharibifu uliotokea kwa gari dogo walilokuwa wamepanda askari na jinsi lilivyoburuzwa na basi kwa umbali wa mita 56 kisha kwenda kusimama umbali wa mita 97, kwa hali hiyo umbali kutoka eneo walipogongana hadi basi liliipoenda kusimama ni mita 152. 
Dereva wa Bus alitoroka mara baada ya ajali hiyo kutokea, juhudi za kumtafuta zinaendelea. 
Miili ya marehemu imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya mkoa Dodoma.
Aidha Kamanda MISIME ametoa wito kwa madereva kila mara wawe na udereva wa tahadhari na na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

No comments:

Post a Comment