STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Jennifer Mgendi ajipanga kutoa mpya

 
MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili, Jennifer Mgendi yupo katika maandalizi ya kufyatua filamu mpya, fani anayoifanya kwa sasa sambamba na hiyo ya kumuimbia Mungu.
Akizungumza na MICHARAZO, Jennifer, alisema ameshaandaa miswada mitatu tofauti ya filamu, lakini hajajua ataanza kuirekodi ipi ili kuwapa burudani mashabiki wake.
Jennifer aliyewahi kutamba na filamu kadhaa ikiwamo Joto la Roho, Teke la Mama Chai ya Moto, alisema kazi ya kurekodi filamu hiyo mpya itafanywa hivi karibuni kwa kushirikisha wasanii nyota wa Bongo Movie na yeye akiwamo ndani ya kazi hiyo.
"Nipo katika maandalizi ya kuanza kurekodi filamu mpya, lakini sijajua nitaanza na ipi kwa sababu mikononi ninazo kazi tatu tofauti," alisema Jennifer aliyejipatia umaarufu mkubwa kupitia nyimbo kadhaa za Injili.
Baadhi ya nyimbo zilizompaisha mwanadada huyo ni pamoja na Mchimba Kisima, Nalia, Asante Yesu na nyingine.

No comments:

Post a Comment