STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Owino, Mkude kuwakabili maafande taifa


WEKUNDU wa Msimbazi, Simba leo inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na maafande wa Oljoro JKT, huku kocha wake, Zdravko Logarusic 'Loga', akisema huenda akamtumia beki wake wa kati, Joseph Owino aliyekuwa amekwaruzana naye kwenye mazoezi ya timu hiyo wiki mbili zilizopita.

Loga alikwaruzana na nyota huyo wa Kenya kwenye mazoezi ya timu hatua iliyopelekea kumuweka benchi kwenye mchezo uliopita dhidi ya Rhino Rangers.

Hata hivyo Kocha huyo alimaliza matatizo na mchezaji huyo na amemjumuisha kwenye kikosi kilichokuwa kikijiandaa na mchezo wa leo dhidi ya JKT Oljoro, utakaochezwa uwanja wa Taifa huku kiungo Jonas Mkude aliyekuwa akitumikia adhabu ya kadi nyekundu akiwa huru naye kushuka dimbani.

Loga alisema kuwa hakuna tatizo ndani ya kikosi chake na kila mchezaji ana nafasi ya kuwemo kwenye kikosi cha leo.

Alisema kuwa Owino anaweza akacheza lakini ataangalia leo asubuhi wachezaji watakuwa kwenye hali gani ambapo Simba inahitaji ushindi ili kuweza kuwafukuzia wapinzani wao waliopo nafasi tatu za juu.

Simba ipo nafasi ya nne na pointi 27, nyuma ya Mbeya City yenye pointi 31 ambayo kesho itapapatena na Yanga yenye pointi 32 katika pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa.

Vinara wa ligi hiyo Azam wenye pointi 33 wikiendi hii hatakuwa na mchezo wowote, ila leo kuna mechi nyingine kali kati ya Ashanti United dhidi ya Mgambo JKT ya Tanga.

No comments:

Post a Comment