STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Libya ndiyo mabingwa wapya wa CHAN-2014

 
LIBYA imeendeleza maajabu ya kushinda michezo yake kwa mikwaju ya penati baada ya usiku huu kunyakua taji la michuano ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) 2014 kwa kuilaza Ghana katika pambano la fainali lililochezwa uwanja wa Cape Town, mjini Cape Town nchini Afrika Kusini.
Timu hizo zilishindwa kutambia katika muda wa kawaida wa dakika 90 na hata zilipoongezwa dakika 30 bado zilishindwa kupenyaza mipira wavuni na kumaliza dakika 120 bila ya kufungana.
Katika hatua hiyo kama ilivyokuwa katika mechi yake ya robo fainali dhidi ya Gabon kisha kwenye nusu fainali dhidi ya Zimbabwe ndivyo ilivyokuwa katika fainali ya leo kwa Libya kuibuka na ushindi wa mikwaju hiyo na kunyakua taji hilo kwa mara ya kwanza wakiwarithi 'ndugu' zao wa Tunisia.
Libya imeshinda taji hilo kwa ushindi wa penati 4-3, ambapo Ghana walipoteza penati mbili za mwanzo kabla ya kujirekebisha na kulazimisha penati kufikia sita na kupoteza ya mwisho iliyowapa waarabu hao taji.
Penati za mabingwa hao zilitumbukizwa kimiani na Faisal Saleh Al Badri, Muataz Mahde Fadel, Ahmed Al Maghasi na Ahmed El Trbi, huku za Mohamed Elgadi na Abdulsalam Omar zikiota mbaya.
Ghana wenyewe walipata penati zao kupitia kwa Attobrah, Saka, Owusu, huku Akuffu, Ainooson na ile ya mwisho ya Tijani zikienda upogo na kuwafanya Black Stars kulikosa kombe hilo kwa mara ya pili katika fainali mbili ilizocheza katika michuano hiyo, mara ya kwanza ikizidiwa kete na DR Congo kule Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment