STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Simanzi! Askari watano wafa ajali Dodoma


TAARIFA zilizotufikia asubuhi ya leo zinasema kuwa, askari watano wamefariki papo hapo baada ya basi la Mohamed Trans, kugongana uso kwa uso na gari ndogo aina ya Toyota Corola katika ajali.
Akizungumza na Radio One, Kamanda wa polisi Mkoani Dodoma, David Misime, amesema kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 9 usiku kuamkia leo katika kijiji cha Namtumba Mkoani Dodoma na abiria waliokuwemo kwenye basi hilo hakuna aliyejeruhiwa.
"Hakuna aliyejeruhiwa kutoka kwenye basi, lakini dereva aliyekuwa anaendesha abiria hao anafahamika kwa jina la Juma Mohamed, amekimbia mpaka sasa haijafahamika yuko wapi, ameongeza kuwa gari ndogo aina ya Toyota Corola imeharibika vibaya na baadhi ya miili ya askari hao imeharibika. " Tumeipeleka miili hiyo hospital kwa ajili ya kuihifahi huku tukisubiri mipango ya mazishi," amesema David.

No comments:

Post a Comment