STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Sunderland yaifumua Newcastle kwao 3-0

Fabio Borini scores form the penalty
Sunderland wakijipatia bao lao la kwanza kwa mkwaju wa penati
MABAO matatu yaliyofungwa na Fabio Borini kwa mkwaju wa penati na mengine mawili ya kila kipindi yameiwezesha Sunderland kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya mahasimu wao Newcastle United.
Newcastle waliokuwa nyumbani walikumbana na kipigo hicho baada ya Borini kufungwa bao la mkwaju wa penati dakika 19 kabla ya Adam Johnson kuongeza la pili dakika nne baadaye na kuifanya Sunderland kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao hayo.
Kipindi cha pili pamoja na wenyeji kujaribu kutaka kurejesha mabao hayo, hali ilikuwa ngumu kwao kwa kufungwa bao jingine la tatu kupitia kwa Jacky Colback katika dakika ya 80.
Ushindi huo umezidi kuipaisha Sunderland iliyokuwa ikiburuza mkia hadi mwishoni mwa mwaka jana ikikwea hadi nafasi ya 12 toka ya 17 iliyokuwa ikiishikilia baada ya katikati ya wiki kupata ushindi wa 1-0.
Katika mechi nyingine ya mapema iliyochezwa sambamba na ile ya St James Park, West Ham United ikiwa uwanja wa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Swansea City, licha ya kumpoteza mshambuliaji wake nyota Andy Carroll dakika ya 59.
Mabao yote ya wenyeji yalitupiwa kambani na Kevin Nolan katika dakika ya 26 na 45.
Kwa sasa kipute cha ligi hiyo ya England inaendelea kwenye viwanja vingine ambapo MICHARAZO itaendelea kuwajuza.

No comments:

Post a Comment