STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Nigeria washindi wa tatu CHAN 2014

 Nigeria players at CHAN
BAO pekee lililofungwa na Chinonso Obiozor dakika za jioni zimeiwezesha Nigeria kunyakua ushindi wa tatu katika michuano ya fainali za CHAN 2014 dhidi ya Zimbabwe iliocheza pungufu kwa muda mrefu baada ya mchezaji wao mmoja Mumbara kulimwa kadi nyekundu dakika ya 17 tu ya mchezo huo.
Nigeria ambayo ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kunyakua taji hilo lililokosa mwenyewe safari hii baada ya waliokuwa watetezi Tunisia kushindwa kutinga fainali za Afrika Kusini, ilionyeshana kazi barabara na wapinzani wao ambao licha ya kucheza pungufu lakini ilionyesha uhai mkubwa.
Obiozor alifunga baoa hilo akimalizia kazi nzuri ya Ejike Uzoenyi na kukifita machozi kikosi hicho cha Stephen Keshi kwa kupata nafasi hiyo licha ya kushiriki kwa mara ya kwanza michuano hiyo.
Saa moja baadaye inatarajiwa kupigwa pambano la fainali za michuano hiyo ambayo itatoa bingwa mpya wa CHAN wakati Ghana itakapopepetana na Libya kwenye uwanja huo huo wa Cape Town.
Timu hizo zilifika hatua hiyo baada ya kupata ushindi wa mikwaju ya penati dhidi ya timu zilizocheza mchezo wa kuwania nafasi ya tatu yaani Zimbabwe na Nigeria.

No comments:

Post a Comment