STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Barcelona yafa nyumbani, Valencia yaifanyizia

FC Barcelona Tickets
VINARA wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona imeshindwa kutamba nyumbani kwake baada ya kunyukwa mabao 3-2 na Valencia licha ya Lionel Messi kuifungia timu yake bao kwa mkwaju wa penati.
Wenyeji walitangulia kupata bao la mapema kupitia kwa Alex Sanchez aliyefunga dakika ya 7 kabla ya wageni kulikomboa dakika moja kabla ya mapumziko baada ya Dani Parejo kufunga.
Kipindi cha pili kilikuwa cha mchakamchaka zaidi kwa timu zote kutafuta mabao zaidi na walikuwa ni Valencia walipopata bao la pili dakika ya 48 lililofungwa na Pablo Piatti, hata hivyo penati ya Lionel Messi katika dakika ya 54.
Paco Alcacer aliifungia Valencia bao la tatu dakika tano baada ya Messi kufunga penati hiyo na kufanya hadi mwisho wa pambano hilo ambalo lilishuhudia Jordi Alba wa Barcelona akitolewa nje ya uwanja  baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu dakika ya 78.
Pamoja na kipigo hicho cha nyumbani Barcelona bado imebaki kileleni ikiwa na pointi 54 sawa na Atletico Madrid na kufuatiwa na Real Madrid yenye pointi 53.

No comments:

Post a Comment