STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 1, 2014

Simba yaua Taifa, Ashanti yanyukwa Chamazi

Amis Tambwe aliyepiga 'hat trick' yake ya pili VPL
Kikosi cha Simba
AMISI Tambwe amedhihirisha nia yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu baada ya jioni hii kufunha 'hat trick' yake ya pili msimu huu wakati Simba ikipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Oljoro JKT.
Mabao hayo yamemfanya mshambuliaji huyo kutoka Burundi kufikisha jumla ya mabao 13 na kuwakimbia Elias Maguli wa Ruvu Shooting na Kipre Tchetche wa Azam wenye mabao tisa kila mmoja wanaomfukuzia katika magoli.
Simba ilitawala pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa kwani ilianza kuandika bao la kwanza dakika ya 12 tu kupitia Jonas Mkude kabla ya Tambwe kuanza vitu vyake kwa kufunga mabao mawili yaliyofanya Mnyama aende mapumziko wakiongoza 3-0.
Tambwe laifunga bao la kwanza kwake na la pili kwa Simba dakika ya 24 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 29 na kuja kupiga 'hat trick' yake ya pili baada ya ile ya kwanza alipoifumua Mgambo kwa magoli yake manne mwaka jana.
Bao hilo la tatu kwake na la nne kwa Simba lilifungwa katika dakika ya 52 akiunganisha krosi ya winga Haruna Chanongo kablka ya kutolewa baadaye na nafasi yake kuchukuliwa na Abdulhalim Humud 'Gaucho'.
Kwa ushindi huo Simba imefikisha pointi 30 na kuendelea kusalia nafasi ya nne nyuma ya Mbeya City ambayo kesho itaikabili Yanga wenye pointi 32 katika pambano jingine linalosubiriwa kwa hamu.
Oljoro inayonolewa na kocha wa zamani wa Coastal Union, Hemed Morocco ilikosa mabao mengi ya wazi katika pambano hilo na hasa kwa mashambuliaji wake Shija Mkina aliyewahi kung'ara na Simba.
Tofauti na mechi yao ya Mgambo, leo Amisi Tambwe alipewa mpira wake na mwamuzi Nathan Lyimo mara baada ya mchezo huo kuisha kwa kupiga hat trick ambayo inakuwa ya tatu, nyingine ilipigwa na Abdalla Juma wa Mtibwa Sugar.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo uliochezwa uwanja wa Chamazi, Ashanti United ilijikuta ikikandikwa mabao 2-0 na Mgambo JKT iliyokuwa chini ya kocha wake mpya Siame aliyempokea Mohammed Kampira.
Kwa ushindi huo Mgambo imefikisha pointi 9, lakini bado imeng'ang'ania mkiani kwa kuzidiwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa dhidi ya Prisons ambayo ina michezo miwili mkononi baada ya pambano lao la kesho dhidi ya Coastal Union kuahirishwa kutokana na tatizo la uwanja wa Sokoine-Mbeya.

No comments:

Post a Comment