STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 13, 2014

Tanzania, Ureno, Algeria zapaa orodha ya FIFA, Hispania bado kinara

TANZANIA imepanda kwa nafasi mbili katika orodha ya ubora wa viwango vya soka duniani kutoka nafasi ya 118 hadi nafasi ya 116, huku Hispania, Ujerumani na Argentina zikiendelea kubaki katika nazo za Tatu Bora kama ilivyokuwa katika orodha ya mwisho.
Kwa mujibu wa orodha mpya iliytotolewa leo la Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) inaonyesha Ureno imepanda kwa nafasi moja toka nafasi ya tano hadi ya nne wakiporomosha Colombia, na Uswisi imepanda kwa nafasi mbili hadi nafasi ya 6 na Uruguay ikiangukwa kwa nafasi moja na kushika nafasi ya 7 juu ya Italia iliyoporomoka kwa nafasi moja pia.
Wenyeji wa michuano ya Fainali za Kombe la Dunia Brazil ilipanda kwa nafasi moja hadi namba 9 na timu inayofungia 10 Bora ya orodha hiyo mpya ni Uholanzi. Timu zilizopo kwenye 20 Bora ukiondoa 10 za kwanza ni pamoja na Belgium,Ugiriki,  Marekani, Chile, Engalnd, Croatia, Bosnia and Herzegovina, Ukraine, Ufaransa na Denmark imefunga dimba.
Kwa upande wa Afrika, Ivory Coast imeendelea kuongoza ikishika nafasi ya 23, huku Algeria ikipanda hadi nafasi ya pili Afrika kwa kukamata nafasi ya 26 na Cape Verde ikiweka rekodi ikikamata nafasi ya 27 na nafasi ya tatu barani Afrika, huku Ghana waliokuwa nafasi ya pili kwa muda mrefu nyuma ya Ivory Coast imeporomoka hadi nafasi ya 4 Afrika na Dunia ya 37.
Misri, inakamata nafasi ya 38 duniani na Afrika ikikamata nafasi ya 5 ikifuatiwa na Tunisia, kisha Cameroon, Nigeria, Mali na Burkina Faso    ikifunga dimba la 10 Bora.
Tanzania wenyewe wamepanda kwa nafasi mbili duniani kwa kushika nafasi ya 116 toka 118 iliyokuwa ikikamata awali na kwa Afrika inakamata nafasi ya 33.
Kwa upande wa CECAFA, Uganda inaendelea kuongoza ikifuatiwa na Ethiopia kisha Kenya ndipo Tanzania , Sudan, Burundi, Rwanda, Eritrea, Sudan Kusini, Somalia na Djibout

No comments:

Post a Comment