STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 13, 2014

Yanga watua Comoro tayari kwa vita

baadhi ya wachezaji wa Yanga wakishangilia moja ya mabao yao
MABINGWA watetezi wa Ligi kuu Tanzania Bara, Yanga wamefika salama mjini Demoni, nchini Comoro tayari kwa mchezo wa marudiano Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji Komorozine siku ya Jumamosi.
Taarifa kutoka nchini humo inasema kuwa kikosi hicho chenye wachezaji 19 wamefika salama tayari kwa mechi hiyo ya mkondo wa pili.
Yanga iliyoondoka mapema leo, imetua nchini humo ikiwa na matumaini makubwa ya kusonga mbele, baada ya kuichapa Komorozine mabao 7-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam Jumamosi iliyopita.
Iwapo Yanga itahitimisha vyema kampeni yake hiyo, itakutana na mabingwa watetezi, Al Ahly mwezi ujao.  

No comments:

Post a Comment