STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Chelsea yaibutua Spurs 4-0 darajani

Et'oo akishangilia bao lake
Samuel Eto'o is congratulated by teammate Branoslav Ivanovic after putting Chelsea ahead
Eto'o akipongezwa baada ya kufunga bao la utangulizi
John Terry
Nahodha John Terry akimpongeza Eto'o
VINARA wa Ligi Kuu ya England ikiwa katika kiwango tishio imeitubua Tottenham Hotspur kwa mabao 4-0 katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo, huku mtokea benchi Demba Ba akifunga mabao mawili dakika za jioni kwenye uwanja wa Stanford Bridge.
Samuel Ot'oo alikuwa wa kwanza kuifungia Chelsea bao dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kabla ya Edin Hazard kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 65 baada ya Younes Kaboul kumchezea vibaya Et'oo kosa lililomfanya alimwe kadi nyekundu na kutolewa uwanjani.
Kocha Jose Mourinho alifanya mabadiliko ya haraka haraka akimtoa Etoo na nafasi yake kuchukuliwa na Demba Ba ambaye hakuwa na ajizi baada ya kufunga mabao mawili katika dakika ya 88 na 90 yaliyotosha kuihakikisha Chelsea kukaa kileleni ikiwa na pointi 66 saba zaidi ya iliyonayo Liverpool na Arsenal zenye 59 kila moja..
Katika mechi nyingine za mapema Cardiff City ikiwa nyumbani iliisasambua Fulham kwa kuicharaza mabao 3-1, Southampton ikiwa ugenini ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Crystal Palace, huku Norwich City na Stoke City ilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1.

No comments:

Post a Comment