STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Tambwe, Mgosi walimwa faini, kisa...!

Tambwe wa Simba
Mgosi
STRIKA nyota wa Simba, Amissi Tambwe amepigwa faini ya Sh 500,000 kwa kuonyesha ishara ya matusi wakati akishangilia bao lake.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema Tambwe alionyesha alama ya matusi kutumia kidole chake wakati anashangilia.

Tambwe alifanya hivyo baada ya kuifungia Simba bao wakati ilipoivaa Mbeya City mjini Mbeya.

Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1, Tambwe raia wa Burundi akiwa ni shujaa wa Simba.

Hadi sasa Mrundi huyo ana mabao 17 akiwa kileleni kwa upachikaji mabao.

Naye, mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Musa Mgosi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kosa la kupiga uwanjani kwenye mechi dhidi ya Ashanti United ambapo vilevile atakosa mechi tatu za ligi. Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa washabiki wake kumrushia chupa za maji kipa wa Mbeya City.

No comments:

Post a Comment