STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

KCCA yakwama kwa Nkana Ligi ya Mabingwa Afrika

The KCC FC team that started against Zambia's Nkana Red Devils in Kitwe
KCCA iliyong'olewa jioni hii kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kukubali kipigo nyumbani
MABINGWA wa Kombe la Mapinduzi, KCCA ya Uganda muda mfupi uliopita imejikuta ikiaga mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na Nkana Red Devils ya Zambia katika mechi ya marudiano iliyochezwa jijini Kampala Uganda.
KCCA ilipata sare ya mabao 2-2 ugenini wiki iliyopita mjini Lusaka, ilijikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0 kabla ya kulirejesha na kuonekana kama ina nafasi ya kusonga mbele kabla ya kuruhusu bao la ushindi la wageni linalowafanya Waganda hao kung'oka kwa jumla ya mabao 4-3.
Washindi wa mchezo huo, Nkana sasa itavaana na Zamalek ya Misri katika mechi ya mkondo unaofuata baada ya jana Wamisri hao kulazimishwa sare ugenini ya bila kufungana na Kabuscorp ya Angola na kufuzu kwa jumla ya bao 1-0 kwa vile mechi iliyopita Zamalek ilishinda nyumbanio bao 1-0.

No comments:

Post a Comment