STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Timu ya Babi, UiTM yazidi kuzama Malaysia

Photo: Thamani.yangu na uwezo .wangu na nithamu yangu ndio inayonifanya .nipewe ukepten..ndani ya nchi na nje ya .nchi..nawatakia kila la heri YANGA..
Abdi Kassim (kushoto wa kwanza) akiwa na utepe wa unahodha katika timu yake uya UiTM
TIMU ya UiTM ya nchini Malaysia anayoichezea kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' imeendelea kuwa urojo katika Ligi Kuu ya nchi hiyo baada ya jana kukubali kipigo cha tatu mfululizo kwa kufungwa na 'vibonde' wa ligi hiyo Perlis.
Babi aliyekuwa nahodha katika mchezo huo, aliishuhudia UiTM ikilambwa mabao 2-1 katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja wa Darul Aman mjini Alor Setar.
Hicho kilikuwa ni kipigo cha tatu mfululizo kwa timu hiyo, kwani baada ya kushinda mechi yao ya kwanza dhidi ya Kuala Lumpur kisha kutoka droo na Johor, ilijikuita ikifungwa mechi mbili mfululizo kabla ya jana kuotewa tena na kuifanya timu hiyo isaliwe na pointi zake nne ikiwa nafasi ya 9 katia ya timu 12 za ligi hiyo.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana baada ya wiki kusimama kwa wiki mbili,timu ya PDRM ilizididi kujizatiti kileleni baada ya kushinda mechi yake ya tano mfululizo kwa kuizamua DRM -Hicom kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini, Sabah ikishinda nyumbani kwa mabao 3-2, PBAPP ikilala nyumba 2-1 na Palau Pinang, Felda United ikitoshana nguvu ya kufunga 2-2 na Johor naNegeri Sembilan na Kuala Lumpur SPA zikitosa sare ya bila kufungana.











































No comments:

Post a Comment