STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Barcelona yazamishwa tena Hispania

Fausto Rossi celebrates
Fausto Rossi akishangilia bao lake lililoizamisha Barcelona leo
Lionel Messi looks upsetBAO pekee lililofungwa na Fausto Rossi katika dakika 17 lilitosha kuizamisha Barcelona ikiwa ugenini wakati ikiumana na Real Valladolid katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania na kuifanya watetezi hao kushindwa kuwaengua kileleni Real Madrid watakaoshuka dimbani kesho.
Barcelona licha ya kuchezesha kikosi chake cha hatari kikiwajumuisha nyota wake kama Lionel Messi, Neymar na wengine ilishindwa kabisa kufurukata mbele ya wenyeji wao na kuwafanya walale na kuwaacha Real wakipumua kileleni wakitofautiana pointi moja, Real wakiwa na 64 na Barca wakiwa na 63 wakitishiwa kuporomoshwa zaidi hadi nafasi ya tatu iwapo Atletico Madrid itakayoshuka dimbani baadaye kama itaibuka na ushindi ugenini dhidi ya Celta Vigo.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jioni hii timu ya Real Betis iliifunga Getafe kwa mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa nyumbani kwa washindi.

No comments:

Post a Comment